Aliekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais ambae kwa sasa ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Mhe Dkt Saada Mkuya Salum na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Mhe Harusi Said Suleiman wakiweka saini hati za makabidhiano huku wakishuhudiwa na Katibu Mkuu Dkt Omar D. Shajak, hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa mkutano Migombani
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na
Mipango Mhe. Dk. Saada Mkuya Salum, amewataka Watendaji wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais,
Zanzibar kuendelea kuwa wabunifu ili kwenda sambamba na maono ya Serikali ya
awamu ya nane ya kutimiza matarajio ya kuwatumikia vyema wananchi.
Dkt. Mkuya ameyasema hayo wakati wa
makabidhiano ya ofisi baina yake na Waziri mpya wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa
Rais Mhe, Harous Said Suleiman kufuatia mabadiliko ya Mawaziri yaliyofanywa na Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Mwinyi hivi karibuni.
Amesema kwamba wananchi wanamatarajio
makubwa ya Serikali ya awamu ya nane katika utekelezaji wa sera na mipango
mbali mbali ya maendeleo na kwamba ni vyema wafanyakazi kujitahidi kwenda
sambamba na matarajio hayo.
Hata hivyo, Dkt Saada amewakumbusha
watendaji hao pia kujitahidi kuenda na muda kwa kuzingatia wakati katika utekelezaji wa shughuli za kazi mbali
mbali ili kumsaidia waziri Harusi kutimiza vyema majukumu yake.
Amehimiza wafanyakazi hao kumpa
mashirikiano Waziri Harusi kama walivyompa yeye ili aweze kutumiza majukumu
yake kwa wepesi na kuweza kupata mafanikio katika sekta zote mtambuka
anazoziongoza ndani ya wizara hiyo.
Naye waziri mpya wa Ofisi ya Makamu wa
Kwanza wa Rais Mhe. Harusi Said Suleiman, amewaomba wafanyakazi hao kumpa
mashirikiano katika kufanikisha utekelezaji wa shughuli za Ofisi ya Makamu wa
Kwanza wa Rais na ujenzi wa nchi kwa jumla.
Aidha amewakumbusha watendaji hao umuhimu
wa kuendelea kufanyakazi kwa mashirikiano na kuheshimu sheria na taratibu za
kazi kama msingi wa mafanikio kazini.
Bi Harusi amezitaka taasisi zote za ndani
kuhakikisha kwamba zinatayarisha na kutekeleza mpango mkakati katika
utekelezaji wa malengo ya taasizi husika.
Naye Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza
wa Rais Dk. Omar D. Shajak, amemshukuru waziri aliyeondoka Mhe. Dkt Saada Mkuya
kwa usimamizi bora kwa kipindi chote alichokuwepo kwa kutumia umahiri na maono
mapana katika kusimamia sekta zilizopo ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais.
Dkt Shajak amesema kwamba katika kipindi
kifupi alichoiingoza Ofisi hiyo usimamizi wake umeleta ufanisi kwa kutekeleza
mambo mengi likiwemo suala la mabadiliko
ya sheria ya kupambana na dawa za kulevya Zanzibar.
Makabidhiano hayo yamefanyika kwenye ukumbi
wa mkutano wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Migombani
No comments:
Post a Comment