Habari za Punde

Zantel yazindua Ofa ya mwezi mtukufu wa Ramadhan • Wateja kupata maudhui ya kiislamu kwa gharama nafuu

 

Mkuu wa Fedha wa Zantel, Aziz Said Ali akimkabidhi zawadi ya Ramadhan, Rashid Ali Mohamed ambaye ni mwandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Ofay a Ramadhan kwa wateja wa Zantel. Ofa hiyo inalenga kuwapa maudhui ya kiislam kama mafundisho,nasheed,adhana, dua na kuwakumbusha muda wa futari na daku.

Mkuu wa Fedha wa Zantel, Aziz Said Ali (katikati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Ofa ya Ramadhan kwa wateja wa Zantel.Kulia ni Afisa wa Bidhaa, Edwin Byampanju. Ofa hiyo inalenga kuwapa maudhui ya kiislam kama mafundisho,nasheed,adhana, dua na kuwakumbusha muda wa futari na daku.

Kampuni ya Mawasiliano ya Zantel leo imezindua ofa ya mwezi mtukufu wa            Ramadhan ambayo itawapa maudhui mbalimbali ya kiislamu yenye kuimarisha imani zao katika kipindi chote cha mwezi mtukufu kwa gharama nafuu.                                       

Ofa hiyo ni sehemu ya azma ya Zantel ya kuhakikisha inakuwa karibu na wateja wake kwa kutoa suluhu zenye kuboresha maisha kijamii na kiuchumi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Ofa hiyo, Mkuu wa Fedha wa Zantel, Aziz Said Ali alisema ofa hiyo ni mahususi kwaajili ya mwezi mtukufu na kwamba imelenga kusogeza maudhui mbalimbali kwa watumiaji wa Zantel ili kuwasaidia kuufanya mwezi mtukufu kuwa mkamilifu.

 ‘’Zantel inapenda kuwatakia waislamu wote duniani mwezi mtukufu wa Ramadhan.Tunatambua mwezi huu ni muda muafaka wa kuimarisha imani zetu kwa kufanya matendo yaliyo mema pamoja na kufanya swala,” alisema na kuongeza;

“Zantel tumeona ipo haja ya kuungana na Waislamu wote hapa nchini kwa kuleta huduma hii ya Ramadhan ambayo itawapa maudhui mbalimbali yanayoendana na mwezi huu ili kukuza imani yetu pamoja na kuwakumbusha mida ya swala tano za kila siku,” alisema.

Maudhui hayo ni pamoja na Dua, Qaswida za Ramadhan ‘Nasheed’, Swala za Taraweeh pamoja na jumbe za sauti kuwakumbusha muda wa daku na Futari. Ukijiunga na huduma hii utapata SMS tano za kukumbusha muda wa swala kwa siku.

Kwa upande wake, Mkuu wa Masoko wa Zantel, Rukia Iddi Mtingwa alisema wateja wanaweza kupata ofa hiyo kwa njia ya simu mahali popote jambo litakalowasaidia kuwa imara kiimani muda wote.

“Lengo letu ni kuhakikisha huduma hii inamnufaisha kila mtu na ndio maana tumehakikisha inapatikana kwa gharama nafuu sana. Kwa Shilingi Mia moja tu (Tsh 100) kwa siku, mteja wetu ataweza kupata taarifa zote hii ambayo itamsaidia kutimiza ibada zake katika mwezi huu mtukufu.”

Ili kupata huduma hii mteja wa Zantel atapiga namba fupi ya 15582 na atafuata maelezo kisha Chagua Ofa ya Ramadhan.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.