Habari za Punde

Tanzania na India Kuja na Mapinduzi Makubwa Kwenye Utamaduni.


Na John Mapepele.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amesema  kuwa Tanzania na India zinakwenda kupitia na kuboresha mikataba ya mashirikiano ya awali  kwenye eneo la Utamaduni na Sanaa iliyojiwekea  mwaka 1984 ili  kuiboresha iweze kuleta mapinduzi makubwa na ya haraka kwa faida ya pande zote.

Mhe, Mchengerwa ameyasema haya leo Juni 17, 2022 akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Hassan Abbasi wakati alipotembelewa ofisini kwake na Balozi wa India nchini Mhe.  Binaya Srikanta Pradhan na kufanya mazungumzo ya kuendeleza mashirikiano kwenye sekta hizo.

Aidha, amesema mambo mengi yalikubalika   baina ya nchi zote mbili hususan  kuendelea kwa tamaduni  pia  kumekuwa na mambo mengi ambayo yameandikwa ambayo kuna haja ya kufanya mapitio.

Ameongeza  kuwa katika maongezi hao  wamekubaliana kuwa  na kituo maalum cha kuandaa filamu ambacho kitatumika kwa nchi za Afrika mashariki ambapo  baadhi ya wasanii kutoka India  watashiriki moja kwa moja kwenye eneo hili.

Pia amesema eneo jingine  kubwa ambalo wamejadili  ni kuhusu umuhimu wa  wa kufanya mkutano mkubwa kuhusu bahari ya Hindi ambao utajumuisha nchi hizo  mbili.

Amesema tamasha hilo litasaidia kuonyesha historia za nchi zote zilikotoka zilipo na zinakoelekea

Aidha, amesema  bahari ya Hindi imebeba historia kubwa ambayo tayari watafiti kutokana  India na Tanzania wamefanya utafiti hivyo ni muhimu  kuutumia utafiti huo kwa faida ya nchi zote.

Naye  Mtaalam  na Mtafiti  Arindam Mukherjee ambaye ameambatana  na Mhe. Balozi amefafanua kuwa tafiti zinaonesha kuwa  Bahari ya Hindi ilikuws ikitumika kwa miaka mingi kufanya biashara  ambapo yapo baadhi ya maeneo ambayo yamethibitika yamekuwa yakikaliwa na waswahili na pia kumekuwa na mfanano wa maneno ya kiswahili.

Na John Mapepele.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amesema  kuwa Tanzania na India zinakwenda kupitia na kuboresha mikataba ya mashirikiano ya awali  kwenye eneo la Utamaduni na Sanaa iliyojiwekea  mwaka 1984 ili  kuiboresha iweze kuleta mapinduzi makubwa na ya haraka kwa faida ya pande zote.

Mhe, Mchengerwa ameyasema haya leo Juni 17, 2022 akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Hassan Abbasi wakati alipotembelewa ofisini kwake na Balozi wa India nchini Mhe.  Binaya Srikanta Pradhan na kufanya mazungumzo ya kuendeleza mashirikiano kwenye sekta hizo.

Aidha, amesema mambo mengi yalikubalika   baina ya nchi zote mbili hususan  kuendelea kwa tamaduni  pia  kumekuwa na mambo mengi ambayo yameandikwa ambayo kuna haja ya kufanya mapitio.


Ameongeza  kuwa katika maongezi hao  wamekubaliana kuwa  na kituo maalum cha kuandaa filamu ambacho kitatumika kwa nchi za Afrika mashariki ambapo  baadhi ya wasanii kutoka India  watashiriki moja kwa moja kwenye eneo hili.


Pia amesema eneo jingine  kubwa ambalo wamejadili  ni kuhusu umuhimu wa  wa kufanya mkutano mkubwa kuhusu bahari ya Hindi ambao utajumuisha nchi hizo  mbili.

Amesema tamasha hilo litasaidia kuonyesha historia za nchi zote zilikotoka zilipo na zinakoelekea

Aidha, amesema  bahari ya Hindi imebeba historia kubwa ambayo tayari watafiti kutokana  India na Tanzania wamefanya utafiti hivyo ni muhimu  kuutumia utafiti huo kwa faida ya nchi zote.

Naye  Mtaalam  na Mtafiti  Arindam Mukherjee ambaye ameambatana  na Mhe. Balozi amefafanua kuwa tafiti zinaonesha kuwa  Bahari ya Hindi ilikuws ikitumika kwa miaka mingi kufanya biashara  ambapo yapo baadhi ya maeneo ambayo yamethibitika yamekuwa yakikaliwa na waswahili na pia kumekuwa na mfanano wa maneno ya kiswahili.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.