Habari za Punde

UVCCM IRINGA WAPONGEZA BAJETI KWA KUWAGUSA VIJANA

Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Iringa Arnold Mvamba akiongea na waandishi wa habari katika ofissi ya umoja ya vijana wa ccm mkoa wa Iringa kuhusu bajeti ambayo imetolewa na serikali ya mwaka 202/2023

Na Fredy Mgunda,Iringa. 

UMOJA wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Iringa wameipongeza bajeti ya mwaka 2022/2023 ambayo imewagusa vijana kwa kiasi kikubwa na wananchi wote.

 

Akizungumza na waandishi wa habari mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Iringa Arnold Mvamba alisema kuwa bajeti imewagusa kwenye maslai ya wananchi hasa vijana katika maeneo ambayo Serikali imeondoa ada kutoka shule ya msingi hadi kidato cha sita jambo ambalo linamanufaa na vijana wengi.

 

Mvamba alisema kuwa vijana wengi walikuwa wanakatisha ndoto zao kwa kukosa ada hasa kidato cha tano na sita hivyo serikali kuondoa ada hiyo kutasaidia kuwa na vijana wengi wasomi.

 

Alisema kuwa kufuta ada kwa Wanafunzi wa kidato cha tano na sita kutakuwa kumewapunguzia adha ya wazazi kutafuta ada na sasa watajikita kwenye shughuli za kimaendeleo na kukuza uchumi wa nchi.

 

Mvamba aliongeza kwa kusema kuwa Serikali kwenye bajeti hiyo imeongeza zaidi ya kiasi cha shilingi bilioni 8 kwa ajili ya kuwakopesha vijana kwenye vikundi ili wakuze mitaji yao.

 

Alisema kuwa kufanya hivyo kutasaidia vijana wengi kujiajiri kwa kufanya shughuli zao binafsi ambazo watasaidia kuajiri vijana wengi na kuongeza soko la ajira kwa vijana.

 

Mvamba aliwataka vijana kuchangamkia fursa mbalimbali ambazo zimekuwa zikitolewa na serikali na kuacha tabia ya kulalamika pasipo na sababu muhimu.

 

Aidha mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Iringa Arnold Mvamba alisema kuwa anakasilishwa na vitendo vya ukatili wa kijinsia unaoendelea mkoa wa Iringa na kuwataka vijana wa Iringa kuacha mara moja tabia hiyo.

 

Alisema kuwa vitendo vingi vya ukatili wa kijinsia vinafanywa na vijana na ndio maana vijana wengi wamefungwa miaka mingi jela jambo ambalo sio jema kwa vizazi vijavyo.

 

Mvamba alisema kuwa vijana wajikite kwenye kufanya kazi ili waepukana na vitendo vya ubaki na ulawiti.

 

Alisema kuwa ana mpongeza mkuu wa mkoa wa Iringa Queen Sendinga kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuleta maendeleo kwa wananchi wa mkoa wa Iringa.

 

Alimazia kwa kuwaomba vijana wengi kujitokeza kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi wa chama ili kupata mamlaka ya kuiongoza chama cha mapinduzi CCM kwenye eneo ambalo anaona anafaa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.