Habari za Punde

Katibu Mkuu Bi.Maganga Amtembelea Njane wa Marehemu Mzee Karume Bibi.Fatma Karume Nyumbani Kakwe Zanzibar.

Mke wa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Aman Karume, Bibi Fatma Karume akizungumza na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga wakati alipomtembelea nyumbani kwake Bumbwini Mkoa wa Kaskazini, Zanzibar. Wengine pichani kushoto ni Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Abdallah Hassan Mitawi na Mratibu Mkuu wa Shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) – Dodoma Bw. Khalid Bakar Hamran.

Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Abdallah Hassan Mitawi akizungumza na Mke wa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hayati Shekhe Abeid Aman Karume, Bibi Fatma Karume wakati wa ziara katika makazi yake Bumbwini Mkoa wa Kaskazini, Zanzibar.

Mke wa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hayati Shekhe Abeid Aman Karume, Bibi Fatma Karume akisoma kitabu cha Historia ya Muungano wakati wa ziara ya Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga na ujumbe wake katika makazi yake Bumbwini Mkoa wa Kaskazini, Zanzibar.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga akiagana na Mke wa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Aman Karume, Bibi Fatma Karume baada ya kumtembelea na kufanya mazungumzo katika makazi yake Bumbwini Mkoa wa Kaskazini, Zanzibar. 

Mke wa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Aman Karume, Bibi Fatma Karume akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga na ujumbe wake walipomtembelea katika makazi yake Bumbwini Mkoa wa Kaskazini, Zanzibar.
 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.