Habari za Punde

Makarani wa Sensa wahimiza viongozi wa kaya kutoa elimu juu ya sensa kwa wananchi

 Na Khadija Mgeni

Makarani wa sensa ya watu na makaazi nchini wamewaomba viongozi mbalimbali waliopo kwenye kaya zao kuzidi kutowa elimu juu ya sensa ya watu na makazi kwani ipo haja ya viongozi wa kaya kutowa hamasa zaidi kwa wananchi wao.

Hayo yamesemwa na makarani wakati  wa mahojiano na   wahamasishaji wa sensa kutoka Afisi ya Mtakwimu Mkuu wakati walipofika kwenye ziara ya kuangaliya  mafunzo kwa vitendo katika kaya  mbalimbali za Mkoa wa Mjini Magharibi . 

Aidha waliwasihi viongonzi wa kaya hizo kutoa elimu kwa  jamii  iliyo wazunguka  kwa lengo la kufanikisha sensa hiyo .

Makarani hao wamewasihi wananchi watakapofika katika kaya zao kuonesha ushirikiano mkubwa kwa kuwapatia takwmu sahihi kwa maendeleo ya kaya zao ikiwemo elimu, afya, majengo pamoja na miundombinu ya barabara.

Sambamba na hayo wamewataka wananchi kutoa taarifa sahihi kwa wanakaya pale atakapopata dharura ya kutokuwepo kwenye kaya yake.

Kwa upande wananchi wa kaya zilizodadisiwa kwa njia ya mafunzo ya vitendo  wamesema wako tayari kushirikiana na makarani watakaopita katika kaya zao ili kuweza kuandaa mipango mizuri ya taifa  kwani bila ya takwimu sahihi huwezi kupata mipango ya kimaendeleo kwa maslahi mapana ya nchi.

Pia wananchi hao wameishukuru serikali yao kwa kuandaa kamati ya uhamasishaji ambayo imefanya kazi kubwa ya kutoa elimu kwa jamii na kuwasaidia kujuwa na kuondokana na dhana potofu juu ya sensa.

Nae mratibu wa sensa wilaya mjini ndugu Khamis Abdurahman Msham amewashukuru wanakaya kwa kuonesha mashiriano yao ya dhati hali ambayo imewatia matumaini ya kufanikiwa kwa kiasi kikubwa sensa ya mwaka huu pia kwa upande wa makarani hao wameonesha uthubutu mkubwa wa kufanya kazi kwa uweledi  katika  mafunzo kwa vitendo  sambambana na kutoa wito kwa wananchi kuwa tayari kuhesabiwa wakati utakapo fika.

Tanzania kila baada ya miaka kumi hufanya zoezi la sensa na watu na makazi ili kuweza kupata takwmu sahihi kwa mipango ya maendele zimebaki takiribani siku kumi na moja kufikia kwa sensa ya mwaka huu

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.