
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na mgeni wake Balozi wa Cuba
Nchini Tanzania Mhe. Yordenis Despaigne, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa
mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu leo 1-9-2022.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amekutana na Balozi wa Cuba nchini Tanzania Yordenis Despaigne, aliefika Ikulu Zanzibar kwa ajili ya kujitambulisha.
Rais Dk. Mwinyi aliishukuru Cuba kwa kuendeleza uhusiano na ushirikiano wa muda mrefu kati yake na Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kupitia sekta za elimu na afya.
Alisema Taifa hilo limekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya Zanzibar kutokana na msukumo mkubwa inayotoa kupitia sekta za Afya na Elimu, ambapo pamoja na kutoa msaada wa madaktari pia hutoa fursa za masomo kwa Wanafunzi wa Zanzibar.
Dk.Mwinyi alimueleza Balozi huyo kuwa Zanzibar inahitaji kuongeza uwezo wake katika utoaji wa huduma za Afya kwa kuwa na madaktari na Manesi baada ya Serikali kujenga Hospitali 10 kutoka katika kila Wilaya na hivyo akabainisha umuhimu wa kupata fursa za mafunzo.
Aidha, Dk. Mwinyi alisema Zanziabr itaendeleza uhusiano na ushirikiano uliopo kati yake na Cuba katika masuala mbali mbali ya kimataifa.
Nae, Balozi wa Cuba nchini Tanzania, Yordenis Despaigne alisema Cuba inajivunia uhusiano na ushirikiano wa Kihistora kati yake na Zanzibar na Tanzania kwa ujumla, na kuahidi kuuendeleza, ili kusaidia juhudi za Serikali katika utoaji wa huduma na kuimarisha uchumi.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza mgeni wake Balozi wa Cuba
Nchini Tanzania.Mhe. Yordenis Despaigne, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa
mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu leo 1-9-2022
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimkabidhi zawadi ya Mlango wa Zanzibar
mgeni wake Balozi wa Cuba Nchini Tanzania Mhe. Yordenis Despaigne, baada ya
kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
leo 1-9-2022
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa zawadi ya picha na mgeni wake Balozi wa Cuba Nchini Tanzania Mhe. Yordenis Despaigne, baada ya
kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
leo 1-9-2022
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na mgeni wake Balozi
wa Cuba Nchini Tanzania Mhe. Yordenis Despaigne, baada ya kumaliza mazungumzo
yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 1-9-2022.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na mgeni wake Balozi wa Cuba
Nchini Tanzania Mhe. Yordenis Despaigne, baada ya kumaliza mazungumzo yao
yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 1-9-2022
No comments:
Post a Comment