Habari za Punde

Jamii yaaswa kuondokana na dhana kwamba watoto yatima ni mzigo

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Zanzibar ‘Nuru Foundation’ ambaye pia ni mke wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mama Zainab Kombo Shaib akiwa katika picha ya pamoja na Watoto  Yatima wakati alipotembelea na kugawa msaada kwa watoto hao huko Skuli ya Donge Mchangani leo Tarehe 11.09.2022. Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar 

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Zanzibar ‘Nuru Foundation’ ambaye pia ni mke wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mama Zainab Kombo Shaib akizungumza na  Wazazi wa Watoto  Yatima wakati alipotembelea na kugawa msaada huko Skuli ya Donge Mchangani leo Tarehe 11.09.2022. Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Zanzibar ‘Nuru Foundation’ ambaye pia ni Mke wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mama Zainab Kombo Shaib akimuuliza hali Bi Mboja Machono Ali wa Kijiji cha Kandwi  Kaskazini A Unguja akiwa amembeba mtoto wake  Asya Kheir Ali . Bimboni ni miongoni wa wanakijiji hicho  wanaoishi katika mazingira magumu. Mama Zainab alikuwa na ziara ya kutembelea watoto yatima na wanawake wanaoishi katika mazingira magumu huko Kaskazini Leo tarehe 11.09.22 . Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Zanzibar ‘Nuru Foundation’ ambaye pia ni mke wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mama Zainab Kombo Shaib akiwa amembeba mtoto Asya Kheir Ali wa Kijiji Cha Kandwi Kaskazini A’ Unguja ambaye wawazi wake wanaishi katika mazingira magumu. Mama Zainab alikuwa na ziara ya kutembelea watoto yatima na wanawake wanaoishi katika mazingira magumu huko Kaskazini Leo tarehe 11.09.22 . Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

Na Mwandishi Wetu 

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Zanzibar Nuru Foundation Mama Zainab Kombo Shaib, ameikumbusha jamii kuondoa dhana kwamba watoto yatima ni mzigo na lazima kutambua kwamba upo wajibu wa kuwalea kwa pamoja na kuwapa kila aina ya matunzo wanayostahiki ikiwemo elimu.

Mama Zainab ambaye pia ni Mke wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar ameyasema hayo huko  Donge Mchangani Kaskazini ‘A’ Unguja alipokuwa akigawa msaada chakula kwa watoto yatima na  wanawake wanaoishi katika Mazingira Magumu wilayani humo.

Amefahamisha kwamba kwamba kufanya hivyo ni hatua muhimu ya kuwafanya watoto waliofiwa na wazazi wao kuishi kwa furaha na kuendelea kupata matunzo na huduma mbali mbali kutoka kwa jamiii.

Amesema kwamba jumuiya ya Nuru Foundation inayojishughulisha na kuwasaidia mayatima na wanawake waliokwenye mazingira magumu na kwamba pia ni wajibu wa kila mmoja katika jamii kutimiza wajibu wa kuelemishana katika kuwatunza na kuthamini watoto mayatima.

Mama Zainab amewataka wazazi na walezi wenye watoto mayatima kuhakikisha kwamba hawabaki nao majumbani kimya kimya na badala yake kuwasajili  na kuwatolea taarifa zao kwa usahihi katika taasisi na jumuiya za namna hiyo ili iwe rahisi kuwapatiwa misaada ya mahitaji yao.

Ameonya tabia ya baadhi ya wanawake kujisahau na kuwapoa manyanyaso watoto yatima baadala ya kuwapatia haki zao ikiwemo elimu, makazi na nyenginezo za msingi ili maisha yao yaweze kuwa bora.

Naye Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma amesema kwamba watoto mayatima ni kundi kubwa lililopo ndani ya jamii  linalohitaji kusaidiwa hivyo jumuiya ya Nuru Foundation inafanya jambo jema kuisaidia serikali katika kuwapatia huduma watoto wa aina hiyo.

Amefahamisha kwamba hatua ya kuwasaidia watoto hao ni muhimu kuendelea kufanyiaka kwa kuwa ni kuunga mkono juhudi za serikali kwa vile pekee haiwezi kufanya kila kitu .

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na watoto Bi Abeda Rashid Abdalla, amesema kwamba shughuli za taasisi kama Nuru Foundation ni muhimu hasa katika kuwasaidia kuwapunguzia mzigo wanawake ambao ndio wanaobeba jukumu kubwa la kuwalea mayatima.

Kwa upande wake Mratibu wa Watoto mayatima wa Mko awa Kaskazini Unguja Mwajuma Kali Makame ameshukuru ujiyo wa Viongozi wa Jumiya hiyo ulioambatana na Uongozi wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na watoto na kusema kwamba inatoa fikra mpya katika kuendelea na jitihada za pamoja ya kuwatunza na kuwalea watoto yatima na wanawake wenye mazingira magumu.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.