Habari za Punde

Kongamano la Nishati safi ya Kupikia linalotarajiwa Kufanyika Mwaka Huu Novemba 1 na 2 Mwaka huu ili kupunguza vifo vinavyotokana na mfumo wa kupumua hususani wanawake

Na.Mwanajuma Abdi -Dar es Salaam.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeri rasmi katika kongamano la Nishati safi ya Kupikia litalofanyika Novemba Mosi na Pili mwaka huu ili kupunguza vifo vinavyotokana na mfumo wa kupumua hususani wanawake.

Amesema kongamano hilo litazungumzia hali ya sasa ya matumizi ya nishati ya kupikia na ufahamu wake, kubadilishana uzoefu na fursa zilizopo pamoja na changamoto kwa kutumia sera, sheria na masuala ya kodi katika kufikia matumizi salama ya nishati.

Akizungumza na wandishi wa Habari jana, Dar es Salaam Waziri wa Nishati Januaruy Makamba amesema kongamano hilo litawashirikisha wadau kutoka serikalini na sekta binafsi, litafanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere.

Alisema watanzania  33,000 wanakufa kwa mwaka, kutokana na magonjwa ya kupumua kutokana na hewa  ya sumu wanayoimeza katika mapafu yao inayotokana na moshi wakati wa kupika chakula kwa kutumia kuni na mkaa.

Alisema athari ni kubwa kwa akinamama na watoto wenye chini ya umri wa miaka mitano, ambao mara nyingi huathirika  wakati wa wanapopika, hivyo  moshi wa nishati hizo huwaathiri kiafya.

Alieleza asilimia 72 ya nishati yote nchini inatumika kwa kupikia majumbani, ambapo asilimia nane ya watanzania ndio wanaotumia nishati safi isiyotoa moshi, huku asilimia  63.5 ni nishati kwa kutumiua kuni na asilimiza zaidi ya 26 ni makaa.

Waziri Makamba alisema hali hiyo inachangia kupata magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo la mfumo wa kupumua na baadae kusababisha vifo, hivyo ili kukabiliana na hali hiyo Wizara ya Nishati imetenga shilingi Milioni 500 katika Bajeti yake ya mwaka huu kwa ajili ya kukabidhiwa Wakala wa Nishati Vijijini  (REA) kwa kuhamasisha matumizi ya nishati salama.

Alisema REA ndio taasisi itayosimamia jambo hilo, kwa lengo la kuboresha na kuondoa mzigo katika sekta ya afya nchini, na kukuza shughuli za kijamii kwa kuongeza fursa za biashara na ajira,  kuwezesha ustawi wa wanawake na ushiriki wao katika shughuli za maendeleo kikamilifu.

Pia wamejipanga kuimarisha mifumo ya kisera, kisheria, kiutawala,  na kikodi ili kuwezesha watanzania kuondokana na nishati hiyo inayoathiri afya zao.

Nae Daktari Bingwa wa Mapafu Dk. Pauline Chale alisema matumizi ya nishati isiyosalama ya kuni, mkaa na mabaki ya wanyama na mimea yanachangia kuongezeka kwa magonjwa ya mapafu kutokana kutoa moshi wenye sumu za aina ya kemikali 200 ikiwemo Nitrogen dioxide gas.

Alisema moshi huo husababisha magonjwa ya kansa ya koo, mapafu, na kushindwa kupumua ambapo kusababisha watu karibu bilioni 1.6 duiniani wanapoteza maisha kutokana na matumizi ya nishati ya kupikia isiyosalama.

Nae Mkurugenzi Mkuu wa REA Mhandisi Hassan Said alisema atahakikisha maeneo yote ya vijijini yanapata nishati salama ya kupikia, ambapo ndio lengo la serikali katika kupata vipimo vya maendeleo ya nchi na kwa mwaka huu kutakuwa na uhamasishaji wa hali ya juu.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.