Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman , akimkaribisha waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stergomena Tax alipowasili ofisini kwa Makamu Migombani mjini Zanzibar kujitambulisha kufuatia uteuzi wake wa hivi karibuni. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Kitengo cha habari.).
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
Mhe. Othman Masoud Othman , (kulia) akizungumza na waziri wa Ushirikiano wa Afrika
Mashariki Mhe. Stergomena Tax alipofika ofisini kwa Makamu Migombani mjini Zanzibar
kujitambulisha kufuatia uteuzi wake wa hivi karibuni. (Picha na Ofisi ya Makamu
wa Kwanza wa Rais Kitengo cha habari.).
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
Mhe. Othman Masoud Othman , (kulia) akizungumza na waziri wa Ushirikiano wa
Afrika Mashariki Mhe. Stergomena Tax alipofika
ofisini kwa Makamu Migombani mjini Zanzibar kujitambulisha kufuatia
uteuzi wake wa hivi karibuni. Kulia kwa
waziri ni Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar Maryam Haji Mrisho .(Picha
na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Kitengo cha habari.).
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, ameitaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikikiano wa Afrika Mashariki kuongeza uelewa kwa wataanzania kuwezesha kuyafahamu masuala mbali mbali muhimu yanayoendelea katika jumuiya za Kimataifa na Kikanda.
Mhe. Othman ameyasema hayo ofisini
kwake Migombani mjini Zanzibar alipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stergomena Tax alieyefika Ofisini kwa
Makamu kujitambulisha baada ya uteuzi uliofanywa hivi karibuni na rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Mhe. Makamu amesema kwamba yapo
masuala mengi na muhimu yanayoendelea katika Jumuiya hizo ambayo watanzania wa
kawaida pamoja na viongozi wanapaswa kuyafahamu katika hatua za michakato hadi
utekelezaji wake kwa mafunufaa ya watanzania wote.
Mhe. Othman amefahamisha kwamba
kufanya hivyo pia ni muhimu kwani kutasaidia
wananchi na Viongozi nchini kuzifahamu fursa mbali mbali za kiuchumi na
kimaendeleo zilizopo katika ngazi ya kikanda na kimataifa ili waweze kuzitumia
kwa faida yao na taifa kwa jumla.
Mhe. Othman ametolea mfano wa Jumuiya
ya Kimataifa inayoshughulikia Haki
Miliki za Wabunifu Duniani (WIPO), kwamba zipo fursa nyingi ambazo kutokana na
kukosekana uwelewa kwa wananchi fursa hizo hazitumiki ipasavyo na pia
kukosekana uwakilishi wa kuchangia masuala mbali mbali pale inapohitajika.
Akizungumzia suala la Balozi mbali
mbali zilizoko katika Kituo cha Kenya ambazo uwakilishi wao pia unafikia
Tanzania, kuhakikisha kwamba shughuli na huduma zao wanazotoa zikiwemo za watalii
wainafikia Zanzibar ili nchi kuweza kunufaikia kupitia kuwepo kwao Tanzania.
Naye Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stergomena
Tax, amesema kwamba wizara hiyo itayafanyia kazi maelekezo aliyopewa na kwamba
suala la ushirikishwaji wa wananchi katika kujenga uwelewa litawekewa mpango
maalumu katika utekelezaji wake.
Amefahamisha kwamba hatua hiyo ni muhimu
katika kurahisisha utekelezaji wa masuala mbali mbali yanayotokana na Jumuia za
Kikatanda na Kimataifa ambayo nchi imeridhia itifaki zake na pia kusainiwa na
Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutekelezwa nchini.
No comments:
Post a Comment