NA
OMAR HASSAN – ZANZIBAR 21/11/2022
Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamad
Khamis Hamad amesema Jeshi la Polisi litawashughulikia kwa mujibu wa sharia madereva
wa bodaboda wanaokiuka sharia na taratibu zilisowekwa ikiwa ni pamoja na
kutojisajili kwenye vyama na Jumuiya za waendesha bodaboda.
CP Hamad ametoa kauli hiyo huko Paje
Mkoa wa Kusini Unguja alipokua akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Paje,
Bwejuu na Michamvi katika mkutano wa kusikiliza kero za wananchi zinazojitokeza
katika maeneo yao.
Amesema kutofuata sharia na kutojisajili kwa waendesha bodaboda wengi kunachangia kujihusisha na vitendo vya uhalifu waendesha bodaboda hao na kwamba inakuwa vigumu kudhibitiwa na Jeshi la Polisi kutokana na kukosekana kwa taarifa zao.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Kamishna Msaidizi wa Polisi Richard Tadei Mchomvu ameitaka jamii kubadili fikra ya kupambana na uhalifu badala yake kuchukua hatua za kuzuia uhalifu katika maeneo yao.
Kwa upande wao wananchi wa Maeneo
hayo wamelalamikia videndo vya uvunjwaji wa Sheria vinavyofanywa na waendesha
bodaboda.
No comments:
Post a Comment