RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Hussein Ali Mwinyi amesema ameridhishwa na hatua zilizofikiwa za ujenzi
katika Hospitali mpya ya Mkoa wa Mjini
Magharibi, inayoendelea kujengwa katika eneo la
Lumumba.
Dk. Mwinyi amesema hayo leo katika ziara fupi alipotembelea Hospitali hiyo ili kuangalia maendeleo ya ujenzi wake.
Akizungumza na Viongozi, watendaji na wananchi walioshiriki katika ziara hiyo Dk. Mwinyi alisema amefurahishwa na kasi ya Mkandarasi anaendeleza mradi huo, ambapo hadi sasa hatua za ujenzi zimefikia asilimia 69 ya kazi yote.
Alisema kuna kila sababu ya kujivunia kwa uwepo wa Hospitali hiyo ambayo ni ya aina yake hapa Zanzibar.
Alisema Serikali ina matarajio makubwa kuwa Hospitali hiyo itakamilika ujenzi wake na kuanza kutumika ifikapo mwezi Aprili 2023 , na kuwa Hospitali mbadala katika kuendeleza tiba na kupisha ukarabati mkubwa unaotarajiwa kufanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja.
Aidha , alibainisha azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kuhakikisha kila Mkoa hapa nchini unakuwa na Hospitali ya aina hiyo.
Wakati huo huo, Dk. Mwinyi aliwatoa khofu wajasiriamali wanaojihusisha na kazi za kutengeneza vyombo vya moto ambao wamelazimika kusimamisha shughuli zao na kuhama eneo hilo ili kupisha ujenzi wa Hospitali hiyo.
Aliwathibitishia
Wajasiriamali hao kuwa tathmini kwa
ajili ya malipo yao tayari imefanyika na
wanatarajiwa kulipwa katika kipindi kifupi kijacho.
Aidha, aliwawahikishia kuwekewa miundombinu muhimu katika sehemu yao mpya kazi
Mapema,
Waziri wa Afya Nassor Ahmed Mazrui alielezea
maendeleo ya Kazi za ujenzi wa Hospitali hiyo na kusema kabla Hospitali
hiyo ilitarajiwa kukamilika ujenzi wake mnamo mwezi Januari 2023 , lakini kutokana
na changamoto ya kuibuka kwa Ugonjwa wa
Covid – 19, baadhi ya vifaa vilivyotarajiwa kutumika vilichelewa kufika nchini. Hata hivyo
akabainisha kuwa tayari mahitaji mengi ya vifaa yameshakamilika.
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment