RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Al
hajj Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali ya Zanzibar itaendelea kutatua
changamoto zinazowakabili wananchi wake na kuwafikishia maendeleo ya haraka kwa
kadri ya hali inavyorusu katika kufanikisha malengo iliyojiwekea.
Al hajj
Dk. Mwinyi aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi
na waumini aliojumuika nao pamoja wakati wa sala ya Ijumaa huko Masjid Al –
Swafaa, Kikwajuni - Gongoni, Shehia ya Kisima majongoo, Wilaya ya mjini Unguja.
Leo Disemba 30,2022.
Alisema
tatizo la mtaro linalowakabili wananchi wa eneo hilo ambalo limekuwa kero kubwa
kwao, Serikali italitatua kwa haraka ili kuwapa wepesi wananchi wake wa
kuendelea na masuala ya msingi ya ujenzi wa nchi na maendeleo kwa ujumla.
Sambamba
na hilo Dk. Mwinyi alitumia fursa hiyo kuwanasihi wazazi, walezi, wazee, masheikh pamoja na viongozi wa eneo hilo,
kujenga jamii yenye maadili na iliyoshiba imaani na hofu ya kumuogopa Mwenyezi
Mungu, ili kupata jamii bora na yenye heshima na mapenzi kwa taifa lao.
“Jamii
kujengwa kimaadili ndio ufumbuzi mkubwa zaidi ili kupata vijana nwenye imani,
uweledi na nidhamu ya uzalendo kwa taifa lao” Dk. Mwinyi akiinasihi jamii ya
Gongoni, Mjini Unguja.
Al hajj
Dk. Mwinyi pia aliwanasihi vijana na waumini
kwenye msikiti huo kusameheana kwa waliokoseana kwa namna yoyote ya maisha yao,
aidha, aliwataka kutubia na kurejesha kwa walivyowachukuliwa wenzao ili kujenga
jamii yenye maadili na imani ya vitendo.
“Vijana
watambue kwamba kudhulumu ni jambo baya sana, yako mambo tutamkosea Mwenyezi
Mungu moja kwa moja tutubieni, lakini yale tunayowakosea, binaadamu wenzetu,
tuwatake msamaha, kama kuna chao tumechukua turudishe, kisha tutubie” Alinasihi
Dk. Mwinyi.
Katika
hatua nyingine Al hajj Dk. Mwinyi aliwahakikishia wananchi hao kwamba
serikali yao bado inapambana na kukabilina na wanaofanya dhulma kuwadhulumu
wenzao na kwamba serikali itawachukulia hatua na kuwawajibisha.
Hivyo,
aliwataka wananchi hao kupunguza matatizo katika jamii yanayotokana na masuala
ya dhulma.
“Huku kwengine tuachieni tutaendelea
kupambana, kupambana kwa maana ya wale wanaofanya dhulma tukigundua
tunawachukulia hatua, lakini dhulma zishakuwa nyingi na nyngine za muda mrefu,
yapo masuala ya nyumba, migogoro ya viwanja, serikali inayatambua hayo”.
Alitahadharisha Dk. Mwinyi
Naye,
Katibu Mtendaji kutoka Ofisi ya Mufti Zanzibar, Khalid Ali Mfaume aliwanasihi waumini wa dini ya kiislamu na
kuwashauri kwa kutofungamana na haki za watu, badala yake kurejesha dhulma
wanazodhulumiana na kudumu kwenye istighfari ili kumcha Mwenyezi Mungu kikweli.
Aidha,
aliwataka waumini hao kuwa na mipaka katika kuchukua haki za watu, sambamba na
kuwataka wajitathmini kwa matendo waliyofanya mwaka 2022 kwa kuukaribisha vyema
mwaka 2023 kwa kumcha Allah (S.W) kwa dhati ya nafsi zao.
Omar
Abdi Abdalla, Khatib wa msikiti wa Masjid Al Swafaa wa Gongoni, alisema dini ya
Kiislaam imeweka mwongozo mzuri kwa waumini wake kufanya toba ili kutubia
makosa waliomkosea Mwenyezi Mungu.l
Akizungumza
kwa niaba ya uongozi wa Msikiti wa Masid Al – Swafaa uliopo Gongoni, Kikwajuni,
Ali Salum Mkweche alisema Wananchi wa eneo hilo wanaungamkono jitihada
zinazofanywa na serikali ya awamu ya nane na kwamba maendeleo anayofanya Rais
Dk. Mwinyi ni makubwa na yakupigiwa mfano kwani kipindi kifupi cha uongozi wake
wameshuhudia maendeleo makuwa katika sekta zote za Elimu, Afya na Maji safi na
salama.
Imetayarishwa na Idara ya Mawasiliano
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment