Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
Mhe. Othman Masoud Othman, akitoa hotuba katika uzinduzi rasmi wa Hifadhi ya Taifa ya Jozani
Ghuba ya Chawa na Hifadhi Hai, ikiwa ni sehemu ya shamra shamra za kutimia
miaka 59 ya Mapinduzi ya Zazibar. Sherehe hizo zimefanyika tarehe 03.01.2023
huko Jozani Kusini Unguja. Picha na Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais Kitengo
cha Habari .
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
Mhe. Othman Masoud Othman, akifungua pazia kuashiria uzinduzi rasmi wa Hifadhi
ya Taifa ya Jozani Ghuba ya Chawa na Hifadhi Hai, ikiwa ni sehemu ya shamra
shamra za kutimia miaka 59 ya Mapinduzi ya Zazibar. Sherehe hizo zimefanyika
tarehe 03.01.2023 huko Jozani Kusini Unguja. Upende wa pili mwenye pazia ni
Waziri wa Kilimo Maliasili na Umwagiliaji Mhe. Shamata Shaame Khamis . Picha na
Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais Kitengo cha Habari .
MKOA WA KUSINI UNGUJA
Makamu wa
Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman
Masoud Othman, amesema uzinduzi rasmi wa
Hifadhi ya Taifa ya Jozani Ghuba ya Chawa na Hifadhi Hai ni ufunguzi muhimu wa fursa nyingi zaidi za
Kiuchumi, Kijamii na Kiikolojia hapa Zanzibar.
Mhe. Othman
ameyasema hayo huko Jozani wilaya ya Kusini Unguja alipozindua rasmi Hifadhi ya
Taifa ya Jozani Ghuba ya Chawa na Hifadhi Hai, ikiwa ni sehemu ya shamra shamra
za kutimia miaka 59 ya Mapinduzi ya Zazibar.
Mhe. Othman
ameitaka jamii wadau na washirika mbali mbali kuhakikisha kwamba hifadhi hiyo
inalindwa ili iweze kutimiza malengo
malengo ya kuisaidia Zanzibar kuongeza pato kutokana na sekta ya utalii
kwa wegeni wengi kuweza kutembelea msitu huo .
Mhe. Makamu
amefahamisha kwamba kwa mujibu wa wataalamu, Hifadhi Hai ina vigezo maalumu
vinavyotumika kuteua eneo, ili kuingia katika Mtandao wa Hifadhi-Hai Duniani.
Amevitaja miongoni
mwa vigezo hivyo kuwa ni kuwepo ushirikishwaji
bora wa wananchi katika mipango na usimamizi wa Hifadhi ya Taifa na kuwepo
Bayoanuwai za aina nyingi na adimu duniani ndani ya msitu husika pamoja na
kuwepo mfumo mzuri wa kugawana faida na hasara miongoni mwa wadau wa
Hifadhi husika.
Mhe. Othman
amesema kwamba kuna umuhimu kwa wadau na na Serikali kuhakikisha kuwa, kwa pamoja wanaendelea
kuvisimamia na kuvilinda vigezo hivyo, kwa hali na mali, na kufuata maelekezo
ya wataalamu.
Aidha
amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inawakumbusha wananchi kwamba, vigezo hivyo
ndiyo misingi mikuu ya uanzishaji na usimamizi wa Hifadhi ya Taifa ya
Jozani-Ghuba ya Chwaka, hata kabla ya kujiunga na Mtandao wa Hifadhi-Hai.
Amesema
kwamba Serikali kwa upande wake inaahidi kuvilinda na kuvisimamia, siyo kwa sababu ya
UNESCO, bali kwa kuamini kuwa, ndiyo miongoni mwa Nguzo za Hifadhi ya Taifa ya
Jozani-Ghuba ya Chwaka na Hifadhi Hai, ambapo pia uwepo wake ni faida kwa
vizazi vya sasa na vijavyo.
Amefahamisha
kwamba kutokana na umuhimu wa kuwepo kwa Hifadhi hiyo sambamba na matakwa ya
kisheria, Serikali ya Zanzibar imeona ni vyema kutangulia kuizindua na baadae
kuendelea na taratibu nyingine za kiutekelezaji kwa faida ya nchi na jamii kwa
jumla .
Aidha Mhe.
Othman ametoa wito kuchukiliwa juhudi za ziada kuupandisha hadhi pia Msitu wa Hifadhi wa
Kimaumbile wa Ngezi-Vumawimbi, ambao kwa kipindi kilichopita ulishidwa kupanda
hadhi kutokana na mapungufu yaliyopelekea kukosekana kwa vigezo muhimu ya
kupandisha hadhi hiyo.
Amesema kutokana na hali hiyo kunahitajika jitihada za makusudi, na Msitu
huo wa Ngezi nao utimize vigezo muhimu vinavyohitajika ili hatimaye uweze
kupanda hadhi ya kiwango cha Hifadhi Hai kama ilivyo Jozani.
Waziri wa
Kilimo, Umwagiliaji na Maliasili
Zanzibar Mhe. Shamata Shaame Khamis, amesema kwamba kuna jitihada kubwa
zilizofanyika zilizosaidia kupatikana kwa hatua hiyo kuupandisha daraja msitu
huo jambo linalochangia kuwepo ongezeko kubwa la wageni wanaotembelea hifadhi
Amefahamisha
kwamba katika mwaka 2022 kuanzia Januari
hadi Novemba, jumla ya wageni 52,666
wametembelea hifadhi hiyo na kuchangia
kuingiza zaidi ya shilingi bilioni . 1.19
huku fedha za kigeni zilizokuswanywa zikiwa zaidi ya dola sitini na nane alfu.
Aidha
amesema katika mwaka 2021, jumla ya wageni 58,902 walitembelea hifadhi hiyo na
kuingiza kiasi cha shilingi bilioni moja
na milioni 56 ikiwa ni ada za kiingilio katika
kipindi cha Januari hadi Disemba mwaka
huo wa 2021 .
Awali Mkuu
wa Mkoa wa Kusini Unguja Rashid Hadid Rashid, amesema kwamba mashirikiano ya
wadau mbali mbali pamoja na kuwepo amani na utulivu nchini kumechangia mkoa huo
kupata fursa ya kuwa na hifadhi hai baada yam situ huo ku8pandishwa daraja jambo
linalochangia kuwepo idadi ya wageni wanaotembelea eneo hilo na kongeza mapato
kwa wananchi na kupunguza ukali wa maisha.
Akisoma
risala ya Ushirika wa Hifadhi hai Jozani
ndugu Awesu Shaaban Ramadhan, amesema kwamba changamoto kubwa inayokabili
ushirika huo ni pamoja na wanajamii
kukosa, uelewa wa sera na sheria na hivyo kuendelea kufanya mambo
yasiyokubalika katika eneo la hifadhi
ikiwemo kukata msitu.
Awali Ofisa
Ikolojia katika Hifadhi hiyo ndugu Habib Abdulmajid , amesema kwamba msitu huo
ni muhimu kwa kuendeleza biashara ya utalii Zanzibar kutokana na kuwa na
vivutio kadhaa kwa watalii.
Amevitaja
vivutio hivyo vya asili kuwa ni pamoja na kuwepo wanyama wengi adimu, ndege, miti
na viumbe wengine ambao wamekuwa
wakiwavutia sana wageni wengi kuja kutembelea msitu huo na kuchangia
kuongeza mapato yatokanayo na biashara ya utalii nchini.
Imetolewa na Kitengo cha Habari Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar leo tarehe 03.01.2022.
No comments:
Post a Comment