Habari za Punde

Rais Dk Hussein Mwinyi akutana Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT pamoja na uongozi wake Ikulu leo

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Bwa. Emmanuel Tutuba na Gavana Mstaafu wa BOT Prof. Florens Luoga na Uongozi wa BOT, wakiwa katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 18-1-2023, alipofika na Uongozi wake kwa mazungumzo na kujitambulisha.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Bwa.Emmanuel Tutuba, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar na Uongozi wa BOT kwa mazungumzo na kujitambulisha leo 18-1-2023, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu na (kulia) Gavana Mstaafu wa BOT Prof. Florens Luoga.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Uongozi wa Benki Kuu ya Tanzania ukiongozwa na Gavana wa BOT Bwa.Emmanuel Tutuba, (kulia kwa Rais) na (lushoto kwa Rais) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Mhe.Dkt.Saada Mkuya Salum.(Picha na Ikulu)   
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Bw. Emmanuel Tutuba (kulia kwa Rais) akiwa na Gavana Mstaafu wa (BOT)  Prof Florens Luoga , alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo na kujitambulisha, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar leo 18-1-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Bw.Emmanuel Tutuba na Gavana Mstaafu wa (BOT) Prof. Florens Luoga, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 18-1-2023.(Picha na Ikulu) 

NA MWASHAMBA JUMA, IKULU

MSARIFU wa taasisi ya Benjamini Mkapa Foundation (BMF), Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameueleza uongozi wa taasisi hiyo, kuendelea kuboresha mifumo ya afya kwenye taasisi yao ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

Aidha, aliutaka uongozi huo kuangalia kwa upana jinsi ya kukamilisha miundombinu ya vifaa tiba pamoja na kuimarisha mifumo ya mawasiliano itakayotoa huduma bora kwa walengwa na kuboresha utendaji kwa kuongeza nguvukazi za ajira ili kutanua wigo kwenye taasisi hiyo.

Dk. Mwinyi aliyasema hayo alipokutana na uongozi na wafanyakazi wa taasisi ya Benjamini Mkapa Foundation Ikulu, Zanzibar.

Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleza ushirikiano wake na taasisi hiyo katika kuimarisha huduma bora za afya pamoja na kupongeza juhudi za BMF katika utendajikazi wake nchi nzima, Bara na Zanzibar.

Mbali na kusifu jitihada zinazochukuliwa na uongozi kwa kuisimamia vyema taasisi hiyo, pia Dk. Mwinyi aliwataka watendaji na wafanyakazi wa BMF kuanzisha bima ya afya kwa lengo la kwenda sambamba na mahitaji ya wananchi.

 “Wenzetu kule Bara washaanza kutoa bima ya Afya na sisi Zanzibar tunakaribia kuanza” Rais Mwinyi aliuelezea uongozi wa BMF.

Katika hatua nyengine Rais Dk. Mwinyi aliwatunuku vyeti, tunzo na fedha taslimu  wafanyakazi waliofanya vizuri kwenye taasisi hiyo kwa kipindi cha utumishi wao pamoja na kuwapongeza.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya BMF, Balozi Tuvako Manongi alisema, bodi yao imeendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi mbalimbali zikiwemo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, wadau wa maendeleo wakiwemo wafadhili kutoka sekta za umma na binafsi pamoja na wachangiaji binafsi katika kuhakikisha wanapata rasilimali fedha.

Naye, Ofisa Mtendaji mkuu wa BMF, Dk. Ellen Senkoro alisema taasisi imekusudia kuvitekeleza vipaumbele vyake vinne ikiwemo kuufanyia tathmini ya Mpango Mkakati uliopo wa taasisi hiyo ili kuongeza ubunifu na wigo wa kuanzisha miradi mipya baada ya mikongwe iliopo kukamilika kwa asilimia 50.

Aidha, alieleza wanaboresha utendaji wa taasisi hiyo kwa kutumia teknolojia za kisasa ili kupunguza gharama za uendeshaji na kufanyakazi kwa weledi na kuongeza kuwa walifanikiwa kutekeleza miradi mikubwa na midogo kwa kipindi cha mwaka 2021/2022 ambayo iliboresha huduma za afya kwa mikoa 25 ya Bara na mitano ya Zanzibar, ikiwemo kuongeza rasilimali watu, kuimarisha miundombinu ya majengo na vifaa tiba pamoja na kukabiliana dhidi ya mapambano ya Ukimwi, kifua kikuu na UVIKO 19.

Hata, hivyo aliahidhi kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya taasisi hiyo na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ili kufanikisha dira ya taasisi yao. 

Taasisi ya Benjamini Mkapa Foundation iliasisiswa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, awamu ya tatu, Hayati Benjamin Mkapa ambayo imebeba maono na sifa za viongozi bora wa Tanzania na bara la Afrika kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.