Pia ametoa wito kwa wabunge kuhamasisha wananchi katika
maeneo yao kushiriki katika biashara hiyo kwa kupanda miti kwa wingi hatua
itakayosaidia katika kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Ametoa kauli hiyo Februari wakati akichangia Taarifa ya
utekelezaji wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira iliyowasilishwa
bungeni jijini Dodoma Februari 01, 2023.
Amesema Wakala wa Huduma za Mistu Tanzania (TFS) sasa
waongeze nguvu katika kuhakikisha misitu yote inayotunzwa, badala ya kukatwa
kwa ajili ya kuni, mkaa au matumizi mengine sasa itatumika katika biashara ya
kaboni
Dkt. Jafo amesema miongoni mwa maeneo ambayo yameanza
kunufaika na biashara ya kaboni ni pamoja na Halmashauri ya Tanganyika mkoani
Katavi ambayo kwa wastani kwa mwaka inapata takriban sh. bilioni 2 hadi 3 hivyo
ametoa hamasa kwa wilaya zingine kuhakikisha wanatunza misitu kwa ajili ya
biashara hiyo.
“Niwaombe ndugu zangu wabunge tupitie kanuni na mwongozo
wa kusimamia biashara ya kaboni hii itasaidia sana hasa jatika kuhakikisha
maeneo yetu na kuona jinsi gani tunayaelekeza hasa katika suala zima la kuvuna
hewa ukaa,” amesisitiza.
Aidha, amesema Waziri Jafo amesema biashara ya kaboni
itagusa TFS ambao wana dhamana ya kuhifadhi misitu na kilimo (agro-forest) kwa wakulima wanaojihusisha
na kilimo cha mikorosho, miparachichi na kahawa.
Katika hatua nyingine Dkt. Jafo amewapongeza wananchi
kwa kuiunga mkono Serikali kwa kuchukulia ajenda ya kuhifadhi mazingira katika
umuhimu wake kwa kuhakikisha wanapanda miti na kuitunza.
Awali akichangia katika taarifa hiyo Mbunge wa Kuteuliwa
Mhe. Liberata Mulamula ametoa wito kwa Serikali kuchangamkia fursa ya kupata
fedha za mabadliko ya tabianchi zinazotolewa na nchi zilizoendelea kwa nchi
zinazoendelea.
No comments:
Post a Comment