Habari za Punde

Mhe.Othman Masoud Atembelea Wafanyabishara Mbalimbali Katika Eneo la Darajani jana Usiku

Na.Rashid Omar.OMKR.  

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amewagiza viongozi wa Manispaa ya Mjini Unguja kuifanyia kazi mara moja changamoto ya uchafu uliopo katika maeneo mbali mbali ya biashara katika maeneo ya mjini hapa.

 Mhe. Othman ametoa agizo hilo alipotembelea biahara mbali mbali zinazoendelea wakati huu waislam wakiwa katika maandalizi ya siku Kuu ya Eid El-fitry wakati Wumini wa dini hiyo  Duniani kote wakielekea kukamilisha Funga ya mwenzi mtukufu wa Ramadhani .

Mhe. Othman alitembelea maduka ya biashara mbali mbali za mahitaji ya wananchi kwa ajili ya sikuu Kuu hiyo ikiwemo , nguo za watoto , viatu, mpazia, kazu za kiume na nyengine  kadhaa kuona hali halisi ya bidhaa hizo , bei na upatikanaji wake  sambamba na kuelewa changamoto za kibiashara zilizopo katika mitaa maarufu ya Mlandege, Mchangani, Mbuyuni na Darajani Zanzibar.

Aidha Mhe . Othman amesema kwamba katika maeneo  mbali mbali aliyotembelea kumekuwa na hali ya uchafu kwa kuwepo taka zilizochanganyika  na maji ya mvua jambo ambalo linapaswa kushughulikiwa haraka ili kuhakikisha mazingira salama ya biashara na shughuli nyengine za wananchi mjini hapa.

Mhe. Makamu amefahamisha kwamba katika kipindi hiki cha maandalizi ya Siku kuu kumekuwa na idadi kubwa ya watu waofika madukani na hivyo kuwepo msongamano mkubwa wa wananchi waotafuta mahitaji yao mbali mbali na kwamba suala la usafi nalo lazima lipewe kipaumbele na wahusika.

Mhe. Othman amesema kwamba ziara hiyo pia imesaidia kuzifahamu changamoto mbali mbali za wafanyabisahara ambazo zinahitaji kufanyiwa kazi katika kujenga ustawi na taswira njema katika kuweka mazingira bora zaidi ya kibiashara hapa Zanzibar.

Amesema kwamba katika ziara hiyo wafanyabiashara kadhaa  wameibua changamoto mbali mbali ambazo serikali inawajibu wa kuzifanyia kazi na  , kutoa maelekezo kwa baadhi ya changamoto hizo ili kuwepo na  utaratibu na mazingira bora ya uendeshaji shughuli za kibiashara nchini.

Mapema baadhi ya wafanyabiashara walileleza kwamba bado kunachangamoto katika suala la ulipaji kodi kutokana na baadhi ya watumishi wa Mamamlaka ya Kodi kuwa na Mtindo wa kuwavizia jambo ambalo linajenga taswira mbaya kati ya mlipa kodi na mamalaka husika.

Aidha wapo baadhi ya wafanyabiashara walioshauri kwamba licha ya kazi kubwa kufanyika lakini kuna haja kubwa kwa mamlaka za bishara kuongeza juhudi za kutoa elimu kwa wananchi katika suala zima ulipaji kodi na wananchi kudai , kuewa na kuchukua risiti baada ya kununua bidhaa

Kwa upande mwengine baadhi ya wafanbyabaiashara walilalamikia hali ya uchafu taka zinaotupwa holela uliochanganyika na maji ya mvua uliopo katika maeneo mbali mbali ya biashara hasa ikizingatiwa kwamba hiki ni kipindi cha mvua jambo ambalo linaweza kuhatarisha afya za wananchi wanofuata huduma kwenye maeneo hayo.

Imetolewa na ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia kitengo chake cha Habaeri leo tarehe 20/04.2023.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.