Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Dkt Aboud Suleiman Jumbe, tarehe 7 Agosti 2023 amefanya ziara katika eneo la ujenzi wa kiwanda Cha Serikali cha Mwani kilichopo Chamanangwe na kujionea maendeleo ya ujenzi wa kiwanda hicho ambapo kwa sasa kimefikia asilimia 90% ya ujenzi kwa hatua ya awali.
Hivi karibuni Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi alitangaza kuja kwa mradi mwengine mpya wa mwani unaofadhiliwa kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Korea (KOICA) na ambao pia, katika mojawapo ya utekelezaji wa program yake, utajenga kiwanda cha ziada cha kutengeneza bidhaa zilizomalizwa (finished products) za mwani. Kiwanda hicho kinatarajiwa pia kujengwa kisiwani Pemba.
No comments:
Post a Comment