Habari za Punde

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Amefunga Mafunzo ya Awali ya Kozi ya Askari wa Uhamiaji Mkoani Tanga

 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea saluti kutoka kwa Kamishina Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala alipowasili  kwenye viwanja vya Chuo cha Mafunzo ya Uhamiaji Kubaga wilayani Mkinga Mkoa wa Tanga kufunga mafunzo ya awali ya kozi Na. 01/2023 kwa Askari wa Uhamiaji , Septemba 29, 2023. Wa pili kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi  Hamad Masauni, kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Kaspar Mmuya na wa nne kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Waziri  Kindamba.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimwagilia mti alioupanda katika bustani ya Majaliwa Square aliyoizindua kabla ya kufunga Mafunzo  ya Kozi Na. 01/2023 ya Askari wa Uhamiaji kwenye viwanja vya Chuo cha Mafunzo ya  Uhamiaji Kubaga wilayani Mkinga Mkoa wa Tanga, Septemba 29, 2023.  Kushoto ni Waziri wa mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Kaspar Mmuya na wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,  Waziri  Kindamba.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea heshima  ya gwaride la Askari wa Uhamiaji kabla ya kufunga  mafunzo ya kozi Na. 01/2023 kwenye viwanja vya Chuo cha Mafunzo  ya Uhamiaji Kubaga wilayani Mkinga Mkoa wa Tanga.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua gwaride kabla ya kufunga mafunzo  ya kozi Na. 01/2023 ya Askari wa Uhamiaji kwenye viwanja vya  Chuo cha Mafunzo ya Uhamiaji Kubaga wilayani Mkinga Mkoa wa Tanga.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua bustani ya Kassim Majaliwa Square kabla ya kufunga mafunzo ya awali ya kozi Na. 01/2023 kwa Askari wa Uhamiaji kwenye viwanja vya Chuo cha Mafunzo ya Uhamiaji Kubaga wilayani Mkinga Mkoa wa Tanga, Septemba 29, 2023. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Kaspar Mmuya na wa pili kushoto ni Kamishina Jenerali wa Uhamiaji, Dkt Anna Makakala.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)




No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.