Habari za Punde

Mhe Othman amnadi mgombea wa ACT Wazalendo uchaguzi mdogo jimbo la Mtambwe

Makamu Mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo Mhe. Othman  Masoud Othman akisalimiana na Mjumbe wa Bodi ya wadhamini wa Chama hicho Mohammed Khamis (Kalipso) wakati Mhe, Makamu alipowasili katika viwanja vya Daya Mtambwe kwa ajili ya ufungaji wa kampeni kuelekea uchaguzi Mdogo wa kiti cha uwakilishio wa Jimbo la Mtambwe Kaskazini Pemba ( Picha na ofisi ya Makamu wa Kwsanza wa Rais wa Zanzibar.)

Makamu mwenyekiti wa ACT Wazalendo Mhe. Othman Masoud Othman akizungumza  huko katika Viwanja vya Daya Mtambwe kaskazini Unguja katika mkutano wa hadhara wa ufungaji wa Kampeni za uchaguzi mdogo wa Uwakilishi wa Jimbo la Mtambwe unaotarajiwa kufanyika Jumamosi  wiki hii. ( Picha na Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman ( kulia), akinyanyua mikono kumuombea kura Dk. Mohammed Ali Suleiman ambaye ni  wa chama cha ACT katika kinyanganyiro cha uwakilishi wa Jimbo la Mtambwe Kaskazini Pemba . Mhe. Othman amemdadi mgombea huyo kwenye viwanja vya Daya Mtambwe katika kutano wa hadhara wa ufungaji wa Kampeni za uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Jumamosi ya Oktoba 28, 2023. ( Picha na ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar).

Makamu  Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Mhe. Othman Masoud Othman akinywa kahawa aliyokaribishwa na wenyeji wake katika Baraza ya wazee Huko Daya Mtambwe wakati Mhe. Othman alipotembelea  baraza hiyo na kuonana na kuwajulia hali wazee wa baraza hiyo.  Kulia kwa makamu ni Mwenyekiti wa Baraza Mzee Hamad Omar Mohammed na Mjumbe wa Baraza hiyo Mzee Mohammed Khatib Juma(makomba) 9    Picha na ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.


Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT- Wazalendo Mhe. Othman Masoud Othman, amesema ni muhimu kwa watu wa Jimbo la Mtambwe watakaoshiriki uchaguzi mdogo wa Kiti cha uwakilishi wamchague mgombea wa chama hicho kwa kuwa ndio sauti ya wanzibari katika kufanikisha mageuzi ya kweli kisiasa na kukuza maendeleo ya kidemokrasia jambo litakalosaidia kufanikisha vita dhidi ya umasikini.

 Mhe. Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, ameyasema hayo huko Daya Mtambwe aliponadi na kumuombea kura mgombea wa uwakilishi wa chama hicho Dk.Mohammed Ali Suleiman katika uchaguzi  mdogo Jiombo hilo utakaofanyika Jumamosi ya tarehe 28 mwezi huu kufuatia kifo cha aliyekuwa mwakilishi wa Jimbo hilo marehemu Habib Mohammed mnamo mwezi Machi mwaka huu.

Amesema kwamba Baraza la wawakilishi ni chombo muhimu kinachotetea haki za wananchi na kwamba mgombea huyo ni chaguo sasa hasa kwa vile ubadhirifu mkubwa umekuwa ukifanywa  katika eneo la manunuzi na kwamba iwapo watamchagua na mbali na kuwa sauti ya wazanzibari waliowengi lakini pia ataweza kulisimamia kwa kulisemea vyema eneo hilo kwa vile ni mbobevu wa taaluma hiyo na kuweza kusaidia vita dhidi ya ubadhirifu wa mali ya umma nchini.

Hivyo , Mhe. Othman amewataka watu wote wa jimbo hilo wenye sifa ya kupiga kura huhakikisha wanajitokeza kwa asilimia mia moja ili kushiriki kumpata mwakilishi halali wa jimbo hilo mwenye uwezo  mkubwa kitaaluma katika kusaidiana kutimiza malengo ya chama hicho ya kuleta mageuzi ya kweli ya kidmokrasia na kuchapuza kasi ya vita dhidi ya umasikini Zanzibar.

Amewafahamisha wananchi hao kwamba Zanzibar  inahitaji kuwepo viongozi makini na majasiri wenye kuacha ubinafsi ambao wataendeleza v yema mapambano ya kuleta mageuzi ya kweli kisiasa na kimaendeleo unaotokana na kuendesha nchi kwa msingi ya ukweli na uaminifu miongoni mwa watendaji na viongozi wenye dhamana mbali mbali.

Amesema kwamba suala la ufisadi katika nchi halihusishi wizi wan a matumizi mabaya ya rasilimali za umma pekee  b ali pia kuwepo utaratibu mbaya wa kuendesha nchi kwa misingi ya kukosa uaminifu na uadilifu jambo ambalo linachangia kuidamirisha nchi kimaendeleo.

Aidha mhe. Othman ameonya tabia na vitendo vya baadhi ya viongozi kutumia vibaya madaraka ya umma walioyopewa na kuendeleza ubinafsi  na hivyo kuwatisha kwa kuwalazimisha wapige kura kukichagua chama wanachokitaka viongozi.

Amesema kwamba kufanya hivyo  mbali na kutumia madara ya umma vibaya lakini pia ni kosa la jinai ambalo haliwezi kufa na kuwaonya wanaofanya hivyo kwamba wanaweza kushitakiwa mahakamani hata katika miaka kadhaa inapopita kwa kuwa sharia za jinai hazina kikomo.

Naye Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama hicho Ismail Jussa Ladhu amewakumbusha wapiga kura hauo wamba Zanzibar inahitaji viongozi wenye uchungu na nchi yao na wamchaguo Mgombe wa ACT Wazalendo katika  jitiohada za kweli za kuleta mageuzi ya kimaendeleo .

Naye Mgombea wa ACT- Wazalendo Dk. Mohammed Ali Suleiman ameama kwamba Jimbo hilo la Mtambwe ni Jimbo mama katika harakati za mageuzi na kwamba ni muhimu kuendeleza jitihada za viongozi mbali bali kwa kumchagua yeye kuendeleza jitihada hizo.

Mhe Othman Mapema amefanya mazungunzo na viongozi mbali mbali wa Jimbo hilo huko Katika Ofisi za ACT-  zilizopo Daya Mtambwe, kutembelea na kuzungunza wanabaraza za chama hicho pamoja na kuwajulia hali wagonjwa mbali mbali kisiwani Pemba.

 

Kitengo cha Habari

Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar

Zanzibar.

Oktoba 26,2023

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.