Habari za Punde

Rais Samia Suluhu Hassan ashiriki Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023, Babati Mkoani Manyara

Vijana wa Halaiki wakionesha maumbo mbalimbali wakati wa Maadhimisho ya Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati Mkoani Manyara tarehe 14 Oktoba, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kiongozi wa Mbio hizo Abdallah Shaibu Kaimu wakati wa Maadhimisho ya Kilele cha mbio hizo katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati Mkoani Manyara.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono Vijana wa hamasa wakati alipokuwa akielekea kukagua mabanda ya Maonesho ya Vijana Kitaifa Babati Mkoani Manyara tarehe 14 Oktoba, 2023.

Matembezi ya Vijana yakipita mbele ya Jukwaa Kuu wakati wa Maadhimisho ya Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati Mkoani Manyara 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Doto Biteko pamoja na viongozi wengine wa Serikali wakati akiangalia Vijana wa Halaiki walipokuwa wakionesha maumbo mbalimbali uwanjani wakati wa Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati Mkoani Manyara

Wakuu wa Mikoa pamoja na viongozi wengine wakiwa kwenye Sherehe za mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati Mkoani Manyara 




 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.