Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman, leo Jumamosi Disemba 30, 2023 amehudhuria pia akiwa Mgeni Rasmi wa Hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi wa Ujenzi wa Jengo la Ghorofa Tatu (3) la Skuli ya Msingi ya Kojani, Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Hafla hiyo, ambayo ni sehemu ya Shamrashamra kuelekea Maadhimisho ya Miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, imewajumuisha Mawaziri na Viongozi mbalimbali wa Serikali, Vyama vya Siasa, Dini, Jamii, Sekta Binafsi, Asasi za Kiraia, Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Vikundi vya Burudani na Vijana Wahamasishaji wakiongozwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Mhe. Lela Mohamed Mussa.
Mheshimiwa Othman yupo kisiwani Pemba kwa Ziara ya Siku Tatu, ikijumuisha pia Uzinduzi wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo, akiwa ameambatana na Mke wake, Mama Zainab Kombo Shaib.
Kitengo cha Habari
Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
Disemba 30, 2023.
No comments:
Post a Comment