Na.Mwandishi OMWR.
Mwenyekiti wa Chama cha ACT-
Wazalendo Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba amewataka viongozi wa chama
hicho katika ngazi mbali mbali
kujitahidi kuwa sauti ya wananchi kwa kuibua ip[asavyo matatizo mbali mbali
yananayowakabuili na kuyawasilisha ili serikali iweze kuchukua hatua.
Mhe. Othman ambaye pia ni Makamu wa
Kwanza wa Rais wa Zanzibar ameyasema hayo huko Shakani wilaya ya Magharibi B
Unguja alipofanya majumuisho ya ziara yake ya kuwatembelea wagonjwa, vizuka na
wenye shida mbali mbali ikiwa ni utaratibu wa chama hicho uliowekwa na
mtangulizi wake marehemu Maalim Seif Sharif Hamad.
Mhe . Othman amefahamisha kwamba
katika ziara hiyo ameweza kushuhudia mambo na matatizo na changamoto kadhaa ya wananchi ambayo
amejifunbza kwamba yanahitaji kusimamiwa na viongozi katika ngazi mbali
mbali hasa kutokana na kuona kwamba
ameweza kujifunza kwamba wapo wananchi wengi ambao wanaishi katika maisha duni
sana
Amesema kwamba ni wajubu wa
viongozi kushriikiana ili kuona kwamba matatizo ya wananchi walionayo wanajitahidi
kuandaa mikakati na mipango mbali mbali iliyosahihi na madhubudi na kufanya
kazi ya kuwa sauti ya wananchi katika kuzifikia na kuzitatua changamoto za
wananchi zinazowakabili katika maeneo yao wanayoishi.
Amesema pia ameweza kujifunza na
kushuhudia shida na changamoto za
wananchi zilizopo katika maisha yao ya kila siku ambazo nyengine, sio kwamba
zimeshindikana kutatuliwa, lakini
inatokana na baadhi ya watendaji kutokujali na kufanya kazi zao kwa
kuwajibika kwa umakini katika kuzikabilki shida hizo.
Amewataja waatendaji hao kuwa ni katika ngazi mbali mbali za serikali za
mitaa , shehia na serikali kuu ambapo ingewezekana kuchukuliwa hatua kwa
matatizo ambnayo wananchi wanakabiliana nayo na kuweza kutatutuliwa.
Aidha Mhe. Othman amasema kwamba
hivi sasa Zanzibar wananchi wanaendelea
kukumbwa na tatizo kubwa la maradhi yasioyoambukiza yakiwemo changamoto
ya sukari, mgongo na mifupa pamoja na kupooza jambo ambalo ni maradhi yanahitaji
kinga zaidi kuliko tiba.
Amesema kwamba maradhi haya
yanahitaji kinga zaidi, lakini pia
yanapotokea bado matibabu yake ni changamoto zaidi kwa wananchi hasa katika
utumiaji wa dawa kwa kuzingatia utaratibu sahihi kama inavyoelekezwa na
wataalamu ili kuwa na uhakika wa kukabiliana na maradhi hayo ipasavyo.
Naye Mwekiti wa Chama hicho katika
Mkoa wa Magharib B Kichama Ali Juma amesema kwamba Zanzibar inaendelea kuwa na
umasikini ambao unaweza ,kuondolewa kwa kuwepo juhudi za pamoja na wazanzibari
kuendelea kuishi vyema.
Aidha wamempongeza mwenyekiti huyo
kutokana kufanya ziara hiyo katika mikoa yote 11 kichama na kutekeleza majukumu
yake mbali mbali kwa ufanisi mkubwa kulingana na malengo ya chama hicho
Mhe. Othman tayari amekamilisha
ziara hizo katika Mkoa wa Kusini Unguja, Mjini Magharib na mikoa miwili ya
Pemba ambapo leo amekamilisha ziara yake hiyo katika wilaya ya Magharib A na B.
Ziara hizo ni mwendelezo wa urithi
uliachwa na Mtangulizi wake Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad ambazo katika uhai wake alizifanya kila ifikapo
mwenzi mtukufu wa Ramadhani kuwatembelea wagonjwa, wenye misiba na shida
nyeingine mbali mbali katika visiwa vya Unguja na Pemba.
No comments:
Post a Comment