Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na bMwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Mwinyi Amepokea Salamu za Pole kutoka kwa Msanii Nassin Abdul Juma Diamond Platinumz Ikulu Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa zawadi maalum na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Wasafi Nasibu Abdul Juma (Diamond Platinumz) baada ya kumaliza kutowa mkono wa pole kufuatia msiba wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Wasafi Nasibu Abdul Juma (Diamond Platinumz) alipofika Ikulu Jijini Zanzibar na Ujumbe wake kwa ajili ya kutowa mkono wa pole, kufuatia msiba wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe wa Kampuni ya Wasafi ukiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Wasafi  Nasibu Abdul Juma (Diamond Platinumz) walipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa ajili ya kutowa mkono wa Pole kufuatia msiba wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amepokea salama za pole kutoka kwa kampuni ya WASAFI inayoongozwa na Mkurugenzi mkuu, Nasib Abdul (Dimond Platinum)

Dk. Mwinyi alipokea Salamu hizo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na kiongozi huyo na ujumbe aliofuatana nao.

Rais Dk. Mwinyi aliushukuru uongozi wa Wasafi uliofika kwa lengo la kumfariji kufuatia msiba wa Baba yake mzazi, Rais Mstaafu wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Mzee Ali Hassani Mwinyi aliyefariki Februari 29, 2024, Dar es Salaam na kuzikwa Kijiji cha Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini, Unguja, Machi, 02 mwaka huu.

Pamoja na mambo mengine pia, Rais Dk. Mwinyi pia aliwashukuru Wasafi kwa kujitoa kwako na kuungamkono juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuyatangaza mazuri yote yanayofanywa na serikali kupitia Sanaa yao ya muziki.

Naye, Dimond Platinum amempongeza Rais Dk. Mwinyi kwa jitihada zake za kuendelea kuwaletea maendeleo makubwa wananchi wa Zanzibar na kusifia jitihada zake wamekua wakizishuhudia kila uchao kupitia mafanikio makubwa kwenye huduma za jamii ikiwemo sekta ya Elimu na Afya.

Alisema hatua za maendeleo zilizofikiwa na Serikali ya Rais Dk. Mwinyi zimevuka malengo ya Ilani ya CCM na Kwenda mbali zaidi.

Dimond Platinum ni nyota maarufu wa Sanaa ya muziki wa “bongo Flavor” Tanzania pia ni mwanamuziki aliefanikiwa kuliteka soko la muziki wa kisasa Afika Mashariki, Afrika na dunia kwa ujumla.   

IDARA YA MAWASILIANO IKULU, ZANZIBAR

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.