Habari za Punde

Wanawake na Uongozi Zanziba


Kwanza tunashukuru sana Mwenyenzi Mungu kwa kutukutanisha tena na katika mwezi huu mtukufu na wa fadhila nyingi, tukiwa tuko hai na wazima.

La pili, sisi watekelezaji wa mradi wa kuwezesha wanawake na jamii kudai haki zao za kidemokrasia na uongozi (SWIL), ZAFELA, PEGAO na TAMWA ZNZ tunapenda kutoa shukurani zatu za dhati kwa wadau mbalimbali ikiwemo taasisi za kiserikali, taasisi za kijamii, jamii, waandishi wa habari, wahamasishaji jamii, viongozi wa dini na taasisi binafsi ambao wamekua nasi pamoja katika utekelezaji wa mradi wa ambao ulianza utekelezaji wake mwaka 2020 hadi na kumalizika mwaka jana 2023.

Kupitia mikutano ya kijamii tumeweza kufikia jumla ya jumla ya watu 11, 129 wengi wakiwa ni wanawake katika mikoa yote ya Zanzibar kupitia mikutano ya uhamasishaji, majadiliano, ufuatiliaji na mafunzo mbali mbali.

Pia mradi umewawezesha wanawake 200 ambao walijengewa uwezo kuhusu masuala ya kidemokrasia, siasa, na uongozi ili waweze kushiriki katika vyombo vya maamuzi.

Aidha, jumla ya waandishi wa habari 199 wamejengewa uwezo wa kuandika habari zinazogusa masuala muhimu kuhusu haki za wanawake na jamii, ambapo jumla ya habari 2,127 ziliandikwa kupitia radio, magazeti na mitandao ya kijamii na kuibua mijadala na kuchochea uwajibikaji wa taasisi mbalimbali ambazo zilisaidia kuleta matokeo chanya katika jamii.

Tumepitia sheria mbali mbali  pamoja na Sheria ya Kadhi 2017, Sheria ya utumishi wa umma (kushiriki katika siasa) No.03 2003, Sheria ya Baraza la Vijana No.16 2013, Sheria ya uchaguzi No. 4 2018, sera ya jinsia ya Tume ya Uchaguzi, Sheria ya utumishi wa umma 2011, Sheria ya vyama vya siasa CAP 258 2002 na Sheria ya Tawala za Mikoa chaNo.7 2014.

Tumeweza kukutana na wahusika mbali mbali wakiwemo Serikali, viongozi wa dini, viongozi wa vyombo vya habari ili kuomba mabadilko ya sera, miongozo, utendaji na uwajibikaji.

Mradi huu ulilenga kumuwezesha mwanamke ambapo ili siyo tu awe kiongozi lakini awe kiongozi bora. Kwa hivyo, tuliweza kuwasimamia ili waweze kufikia lengo hilo ikiwemo pia kuwafundisha sera na haki zao na kuweza kufuatilia haki zao binafsi na haki za wanajamii. Hii tuliifanya kupitia Wahamasishaji jamii (CBs), ambao walijengewa uwezo katika masuala ya uongozi, siasa na Kwa hivyo, waliweza kuibua  changamoto zaidi ya 1,000 za jamii na za mtu mmoja mmoja. Zaidi ya changamoto 771 wameweza kuzichukuliwa hatua na zaidi ya 400 zimeshapatiwa ufumbuzi.

Waandishi wa habari kwa upande wao waliibua viongozi mbali mbali, waliibua maswali mbali mbali. Kwa mfano Nihifadhi ….aliandika habari kuhsusu bi Njuma Ali Juma wa Meli NNe SACCOSS alivyoanzisha na kuipaisha SACCOSS hiyo hadi kuwa na magari yake wenyewe na kutoa mkopo hadi milioni 10. 

 

Mwandishi Khadija Kombo aliandika habari kuhusu muwekekezaji aliyeweka ukuta Michamvi ambapo watu walishindwa kupita na jitihada za wananchi kumkataza ziligonga mwamba. Baada ya kipindi chake kulichotoka kwenye televisheni Mkuu wa Mkoa wa kusini Unguja aliingia kati na kumshauri muwekezaji huyo kuvunja ukuta huo.

 

Tumeweza kuandaa pia sera ya kijnsia , madawati ya kijinsia na taarifa katika vyombo vya habari 11 ambavyo hadi sasa vyombo saba vimeshapitisha sera zake.

Tunashukuru pia tumeaandaa tunzo za umahiri kwa wandishi wa Habari na tumekuwa tukipata washindi.   Jumla ya washindi 35 walipatikana ambapo kati yao wanawake walikua ni 29 na wanaume 6.

Tunatoa Pongezi za dhati kwa Mamlaka za uteuzi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kutambua mchango wa wanawake katika kuleta maendeleo hivyo kuongeza idadi ya viongozi wanawake katika kipindi chake uongozi.

 

 

 

 

Sno

Leadership Position

Men

Women

Total

%age of Women

1

Ministers

12

6

18

33%

2

Deputy Ministers

4

3

7

43%

3

Principal Secretaries (PS)

11

7

18

39%

4

Deputy Principal Secretaries (DPS)

7

5

12

42%

5

Regional Commissioners (RC)

4

1

5

20%

6

Regional Administrative Secretaries (RAS)

4

1

5

20%

7

District Commissioners (DC)

8

3

11

43%

8

Judges

7

4

11

36%

9

Shehas

325

66

391

 17%

 

TOTAL

383

95

478

  

 

Pia katika vyama tumeona mashirikiano na vyama vya siasa, CCM, chama cha ACT kimeandaa sera ya kijinsia na hivyo kuwa na malengo ya kuleta usawa wa kijinsia katika chama.

Hata hivyo, mradi ulikumbana na changamoto kadhaa, ikiwa ni pamoja na upatikanaji mdogo wa takwimu za nafasi za wanawake katika ngazi mbalimbali za uongozi, kukosekana kwa sera na sheria zinazolazimisha usawa wa kijinsia katika sekta zote, baadhi ya viongozi hawazingatii usawa wa kijinsia katika teuzi mbalimbali wanazozifanya pamoja na kukosekana kwa sera ya jinsia katika vyama vya siasa.

Vilevile, mifumo ya upatikanaji wa haki saa nyengine inakuwa ni kikwazo kwa wananchi kupata huduma kwa urahisi. Kwa mfano wale ambao hawana vyeti vya kuzaliwa Pemba.

Kubwa pia ni ukosefu wa kanzi data za wanawake na uongozi kaitka ngazi zote kwa mfano viongozi wa Bodi, wajumbe taasisi binafsi, na data base ya wanawake wanaoweza kuwa viongozi.

Katika kipindi cha utekelezaji wa mradi, tumejifunza umuhimu wa kutumia vyombo vya habari katika kupaza sauti za jamii katika kuibua changamoto zao na kuongeza uwajibikaji wa viongozi, muamko  wa elimu kwa wanawake kuhusu haki zao umeonyesha kuwa unawezesha  kudai na kufuatilia haki zao na Ushirikiano na wadau mbalimbali umethibitisha kuwa muhimu katika kufanikisha malengo ya kijamii.

Kwa kuzingatia yaliyojifunza na mafanikio yaliyopatikana, tunapendekeza yafuatayo:

1. Kuanzishwa kwa kanzidata ya viongozi wanawake waliyoko katika sekta mbalimbali.

2. Kuweko kwa sera na sheria zinazolazimisha usawa wa kijinsia katika sekta zote.

3. Kuwepo kwa mifumo rafiki ya upatikanaji wa huduma za kijamii kwa wananchi.

Mwisho, si kwa umuhimu tunatoa shukurani kwa ubalozi wa Norway nchini Tanzania kwa kufanikisha utekelezaji wa mradi huu, na  tunatoa wito kwa wadau wote wa maendeleo kushirikiana katika kuwawezesha wanawake na jamii kwa ujumla kudai haki zao za kidemokrasia, siasa, na uongozi.

 

Imetolewa na:

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA, ZNZ)

 Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA)

 Jumuiya ya Mazingira, Jinsia na Utetezi Pemba (PEGAO)

 

Na KUSOMWA NA Dkt. MZURI ISSA,

MKURUGENZI TAMWA,ZNZ.

 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.