Habari za Punde

Alhajj Hemed - Amewashukuru Viongozi na Wananchi Waliofika Katika Iftari hiyo na kueleza kuwa mkusanyiko huo unaleta umoja katika jamii.


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amejumuika na Viongozi mbali mbali, waislamu na wanachi wa Mkoa wa Mjini Magharibi katika Iftar aliyoiandaa kwa ajili yao iliyofanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idris Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amejumuika na Viongozi na Wananchi mbali mbali katika Futari aliyoiandaa kwa ajili yao iliyofanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idriss Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.

Akitoa shukurani katika Iftari hiyo Alhajj Hemed amewashukuru Viongozi na Wananchi waliofika katika Iftari hiyo na kueleza kuwa mkusanyiko huo unaleta umoja katika jamii.

Aidha amewakumbusha waumini wa dini ya kiislamu 

kuendeleza tabia ya kuhurumiana na kusaidiana kwa kutoa 

walivyonavyo kwa makundi maalum ikiwemo Mayatima, 

Wazee, Wajane na Watu wenye Ulemavu hasa  katika kipindi 

hichi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

Amewasisitiza wananchi kuendelea kudumisha amani na 

utulivu kabla, wakati na baada ya uchaguzi ili kutoa fursa kwa 

serikali kuijenga zanzibar kimaendeleo.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Idriss Kitwana 

Mustafa amemshukuru Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar 

kwa kuendeleza Ibada hiyo ya kufuturisha ikiwa ni kawaida kwa 

Viongozi na Waumini kufuturishana ndani ya Mwezi Mtukufu 

wa Ramadhani.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.