Habari za Punde

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Philip Mpango Azindua Mbio za Mwenge kwa Mwaka 2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwasha Mwenge wa Uhuru kuashiria uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2025 katika hafla iliyofanyika Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha mkoani Pwani tarehe 02 Aprili 2025.

Wakimbiza Mwenge wa Uhuru kwa Mwaka 2025 wakiingia katika Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha mkoani Pwani tayari kwa kuanza zoezi la kukimbiza Mwenge wakati wa Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2025 uliyofanyika Kibaha mkoani Pwani tarehe 02 Aprili 2025.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akimkabidhi Mwenge wa Uhuru kiongozi wa Mbio za Mwenge kwa Mwaka 2025 Bw. Ismail Ali Ussi mara baada ya kuzindua Mbio hizo katika Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha mkoani Pwani tarehe 02 April 2025.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia wakati wa uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2025 katika hafla iliyofanyika Uwanja wa Shirika la Elimu  Kibaha mkoani Pwani tarehe 02 Aprili 2025.




Kikundi cha Watoto wa Halaiki wakifanya maonesho mbalimbali wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2025 iliyofanyika Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha mkoani Pwani tarehe 02 Aprili 2025.

Kikundi cha Watoto wa Halaiki wakifanya maonesho mbalimbali wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2025 iliyofanyika Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha mkoani Pwani tarehe 02 Aprili 2025.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiagana na Viongozi na Wananchi mbalimbali mara baada ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2025 katika hafla iliyofanyika Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha mkoani Pwani tarehe 02 Aprili 2025.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.