Habari za Punde

TANGAZO LA BARAZA LA MADAKTARI – ZANZIBAR

                                                                   TANGAZO

                                                BARAZA LA MADAKTARI – ZANZIBAR
                      SHERIA YA MADAKTARI NA MADAKTARI WA MENO, NO. 12 YA 1999



             KWA MADAKTARI WOTE.

      Madaktari wote wanaotaka kutoa na wanaotoa huduma Zanzibar (Medical and Dental Practitioners) wanatakiwa kujisajili kwa mujibu wa Sheria ya Madaktari na Madaktari wa Meno, chini ya kifungu cha 10(1) cha Sheria no. 12 ya 1999 . Madaktari wote wanatakiwa kupeleka maombi yao ya usajili kwa BARAZA LA MADAKTARI - ZANZIBAR liliopo Hospitali ya Mnazi Mmoja .

     Ni kosa kisheria chini ya kifungu cha 22 cha sheria hiyo, kwa Daktari yoyote kutoa huduma ya udaktari( medicine, surgery or Dentistry) bila ya kusajiliwa na kupewa kibali na baraza hilo.

     Baraza limo katika mchakato wa kutaka kuwachukulia hatua za kisheria wale wote wanaotoa huduma ya udaktari bila ya kusajiliwa. Baraza linasisitiza kwa wale madaktari wazalendo waliopewa usajili wa muda wafike haraka kwenye Baraza kwa kupatiwa usajili wa kudumu.

    Kwa Mawasiliano:
    Mrajis
    Baraza la Madaktari
     P.o.Box 236
    Tel. 0775045519
    Mnazi Mmoja – Hospital
    Zanzibar.



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.