BARAZA LA MJI WETE
1.
Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2011/2012, Baraza la Mji la Wete lililenga kukusanya TZS 45.6
millioni kupitia vyanzo vyake na hadi kufikia mwezi Machi 2012, Baraza
limekusanya TZS 48.4 millioni sawa na asilimia 106 ya makadirio ya mapato na
kutekeleza malengo yafuatayo:-
a)
Baraza limetengeneza Ukumbi wa
Mikutano wa Jamhuri Hall kwa kutia plasta, rangi, umeme, mafeni na vigae vya
sakafuni.
b)
Limeendelea kuimarisha miradi ya jamii
kwa kusaidia vifaa vya ujenzi na maji katika wadi 7, Kipangani, Selemu, Jadida,
Utaani, limbani, Kizimbani na Bopwe venye thamani ya TZS. 15 milioni.
2.
Mheshimiwa
Spika, shughuli
nyengine iliyotekelezwa na Baraza ni
kushughulikia kazi za matengenezo ya Soko la samaki Bandarini kwa kuunga maji, kutia
rangi na umeme.
3.
Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2012/2013, Baraza la Mji la Wete inakusudia kutekeleza malengo
yafuatayo:-
a)
Kukusanya jumla ya TZS 50 milioni
kutoka katika vyanzo vyake vya mapato
b)
Kuengeza ujazo wa kifusi katika kituo
cha kuegesha gari Wete
c)
Kuendelea na ujenzi wa Ukumbi wa
Mikutano (Jamuhuri Hall)
d)
Ukarabati wa barabara kutoka chinjioni
mpaka Bandarini.
e)
Kuendeleza huduma za usafi katika eneo
la Baraza la Mji wa Wete.
HALMASHAURI YA WILAYA YA WETE
4.
Mheshimiwa
Spika, Halmashauri
ya Wilaya ya Wete kwa mwaka wa fedha wa 2011/2012 ililenga kukusanya TZS 40
milioni kutokana na vyanzo vyake vya mapato na hadi kufikia mwezi Machi 2012,
Halmashauri ya Wilaya ya Wete imekusanya TZS. 59.2 milioni sawa na asilimia 148
ya makadirio na kutekeleza yafuatayo:-
a)
Imekamilisha ujenzi wa Msingi wa Ofisi
ya Halmashauri, jumla ya TZS 15.8 milioni zimetumika.
a)
Halmashauri imetoa msaada wa vifaa vya
ujenzi katika Skuli za Maziwani, Mchangamdogo, Kojani, Daya, Ukunjwi, Mjini
Kiuyu, Ole msingi, Pandani msingi, Bwagamoyo na Fundo. Aidha, Halmashauri ya
Wilaya ya Wete imejenga vyoo vya bei nafuu Mchangamdogo na imetoa elimu ya Afya
na kununua vifaa vya usafi Kojani vyenye thamani ya TZS 5 milioni.
5.
Mheshimiwa
Spika, shughuli
nyengine iliyotekelezwa na Halmashauri
ya Wilaya ya Wete ni kusaidia wananchi waliopata maafa kwa kuunguliwa moto
nyumba zao katika maeneo ya Ole na Mzambarau Takao ambapo TZS 330,000
zimetumika.
6.
Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2012/2013, Halmashauri ya Wilaya ya Wete inakusudia kutekeleza
malengo yafuatayo:-
a)
Kukusanya jumla ya TZS 75 milioni kutoka katika vyanzo
vyake vya mapato
b)
Ujenzi wa Ofisi ya Halmashauri wa
Wilaya ya Wete iliyoko Bahanasa.
c)
Kusaidia huduma za Afya na Mazingira
kwa kutoa mafunzo katika Wilaya ndogo, Kojani.
d)
Kusaidia vifaa vya ujenzi wa madarasa
ya Skuli katika Wadi.
e)
Kununua pikipiki itakayoimarisha
shughuli za ufuatiliaji wa ukusanyaji wa mapato.
HALMASHAURI
YA WILAYA YA MICHEWENI
7.
Mheshimiwa
Spika, Halmashauri
ya Wilaya ya Micheweni katika mwaka wa fedha 2011/2012 ililenga kukusanya TZS
30 milioni kupitia vyanzo vyake vya mapato na hadi kufikia mwezi Machi 2012,
imekusanya TZS 60 milioni sawa na asilimia 200 ya makadirio ya mwaka na
kutekeleza yafuatayo:-
a)
Imeezeka na
kupiga plasta Chinjio la Mziwanda, imejenga choo Konde Mjini, imesaidia
matofali Skuli ya Sekondari Micheweni na imeanza msingi wa Skuli ya Msingi Mawe
Matatu Makangale.
b)
Imenunua vitendea kazi zikiwemo Vespa
mbili.
8.
Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2012/2013, Halmashauri ya Wilaya ya Micheweni inakusudia
kutekeleza malengo yafuatayo:-
a)
Kukusanya TZS 77 milioni kutoka katika
vyanzo vyake vya mapato.
b)
Kujenga ukumbi wa mikutano Micheweni kuanzia
msingi hadi sehemu ya linta.
c)
Kusaidia miradi ya jamii, wanafunzi na
majanga.
d)
Kusaidia ununuzi wa vifaa vya ujenzi
wa kituo cha Afya cha Simai katika eneo la Machengwe.
e)
Kusaidia kazi za kusambaza mabomba ya maji
kijiji cha Kikunguni na Kibubunzi.
f)
Kuongeza
ufanisi kazini ikiwemo kuwapatia wafanyakazi stahili zao, kununua vitendea kazi
vya kisasa na samani.
IDARA YA
URATIBU IDARA MAALUM ZA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR
9.
Mheshimiwa
Spika, Idara
hii ina wajibu wa kusimamia na kuratibu kazi zote za Idara Maalum za SMZ ikiwa
ni pamoja na utekelezaji wa Sera, Sheria na kanuni za Idara Maalum za SMZ,
kusimamia vikao vya Tume ya Utumishi pamoja na Mahkama ya Rufaa za Idara Maalum
ya SMZ. Aidha, inasimamia majukumu ya Kisera ya kuoanisha miundo ya kiutumishi,
maslahi ya maafisa na wapiganaji, kuwajengea uwezo wa kitaaluma na kuratibu
masuala ya michezo na utamaduni ndani ya Idara Maalum za SMZ.
10.
Mheshimiwa
Spika, Idara
ya Uratibu Idara Maalum za SMZ, kwa mwaka wa fedha 2011/2012 iliidhinishiwa TZS
145 milioni kwa kazi za kawaida na hadi kufikia mwezi Machi 2012, Idara hii
iliingiziwa TZS 84.1 milioni sawa na asilimia 58 ya makadirio ya matumizi ya
kawaida na kutekeleza yafuatayo:-
a)
Imefuatilia
kwa karibu shughuli zote za maendeleo na za kawaida zilizotekelezwa na Idara
Maalum za SMZ.
b)
Imefanikisha
vikao vitatu vya Tume ya Utumishi ya Idara Maalum za SMZ.
c)
Imefanikisha
Vikao vitatu vya Mahkama ya Rufaa ya Idara Maalum ya SMZ.
d)
Idara
imewajengea uwezo wafanyakazi wake wawili kwa kuwapatia mafunzo ya muda mfupi
e)
Imenunua
vitendea kazi vipya ili kuboresha ufanisi kazini.
11.
Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2012/1013, Idara ya Uratibu wa Idara Maalum za SMZ imejipangia
kutekeleza malengo yafuatayo:-
a)
Kuendelea
kusimamia na kuratibu kazi za kawaida na miradi mitano ya maendeleo
itakayotekelezwa Idara Maalum za SMZ.
b)
Kufanikisha
vikao vitano vya Tume ya Utumishi ya Idara Maalum za SMZ.
c)
Kufanikisha
vikao vitano vya Mahkama ya Rufaa ya Idara Maalum za SMZ.
d)
Kufanya
mapitio ya Sera, Sheria na kanuni za Idara Maalum za SMZ.
e)
Kuandaa
mipango ya Rasilimali watu na kupitia miundo ya utumishi pamoja na kupandisha
vyeo kwa Wapiganaji.
f)
Kuwajengea
uwezo wa kitaaluma wafanyakazi wa Idara katika ngazi ya Shahada ya Pili, Cheti na
mafunzo ya muda mfupi.
g)
Kukijengea
uwezo wa uzalishaji Kiwanda cha Ushoni cha Idara Maalum za SMZ
h)
Kuhamasisha
shughuli za michezo na utamaduni ndani ya Idara Maalum za SMZ
12.
Mheshimiwa
Spika, ili
Idara ya Uratibu wa Idara Maalum za SMZ iweze kutekeleza majukumu yake kwa
ufanisi, kwa mwaka wa fedha 2012/2013, naliomba Baraza lako Tukufu liidhinishe
TZS 200 milioni kwa matumizi ya kazi za kawaida.
KIKOSI MAALUM CHA KUZUIA MAGENDO (KMKM)
13.
Mheshimiwa
Spika, Kikosi
Maalumu cha Kuzuia Magendo (KMKM) kimeanzishwa kwa Sheria Namba 1/2003 na kina
jukumu la ulinzi na kupambana na shughuli za magendo na uvuvi haramu katika
bahari ya Zanzibar.
14.
Mheshimiwa
Spika, Kikosi
Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM), kwa mwaka wa fedha 2011/2012 kiliidhinishiwa
TZS 6,887 milioni kwa kazi za kawaida na hadi kufikia mwezi Machi 2012, Kikosi
kiliingiziwa TZS 6,082.9 milioni sawa na asilimia 88.3 ya makadirio ya matumizi
ya kawaida na TZS 200 milioni sawa na asilimia 100 kwa matumizi ya kazi za
maendeleo na kutekeleza yafuatayo:-
a)
Kikosi kimewapatia sare na vifaa
Maafisa na Askari wote.
b)
Vyombo vikubwa na vidogo vya doria
baharini vimekuwa katika hali ya utayari na vinaendelea kupata matengenezo
yanayohitajika kila mara.
c)
Kikosi kimefanya matengenezo ya banda
la askari Msuka na Ofisi mpya ya uzamiaji (Diving) Makao Makuu Unguja. Aidha,
ujenzi wa Hospitali ya Kibweni unaendelea katika ghorofa ya kwanza pamoja na
ujenzi wa Laundry. Hanga la kulala askari la kambi mpya ya KMKM Tumbatu limeezekwa.
d)
Chombo KM 204 Miwi na KM 103
vimeshashuka chelezoni baada ya kumaliza matengenezo yaliyokusudiwa.
e)
Vifaa vya uzamiaji vimenunuliwa
vikiwemo suti na mitungi ya gesi. Boti aina ya fibre na mashine yake
imenunuliwa kwa ajili ya usafiri wa wazamiaji.
f)
Ulinzi wa doria umeimarika zaidi baada
ya kupata boti mpya tano za fibre, vile vile vifaa vya mawasiliano (Radio Base
Station) vimenunuliwa.
g)
Kikosi kimeweza kudhibiti utoroshaji wa zao la
karafuu na jumla ya matukio 14 yalidhibitiwa. Pia Kikosi kimefanikiwa kukamata
vitu vifuatavyo:- Mafuta ya Diesel
25,950 Litres, Mafuta ya Petrol 1,790
liters, Sukari 20,250 kgs, kgs 76,800 za mchele na karafuu mbichi 200 kgs.
h)
Kikosi kimewapatia mafunzo Maafisa na
Askari 42 katika fani ya uhasibu, sheria, utawala, afya, manunuzi, taaluma ya
bahari na ufundi.
i)
Vifaa vya upasuaji kwa Hospitali ya
KMKM Kibweni vimenunuliwa.
15.
Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2012/2013, Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo (KMKM) kimejipangia
kutekeleza malengo yafuatayo:-
a)
Kuendeleza kuimarisha nguvu za doria
baharini.
b)
Kuimarisha sehemu ya uzamiaji (Diving)kwa
kununua mashine ya kuhifadhi maisha ya binaadamu chini ya bahari (chamber),
vifaa vya uzamuaji (lifting bag), nguo za kuogelea na mashine ya kujazia hewa
(compressor).
c)
Kuhakikisha wafanyakazi wote
wanawajibika ipasavyo kwa kuwapatia stahili zao
d)
Kuendelea kuwapatia sare na vifaa vya
kulalia Wapiganaji
e)
Kuendelea kuwapatia elimu ya kazi
wapiganaji nje na ndani ya Kikosi.
f)
Kuendeleza matengenezo na ujenzi wa
majengo KMKM katika kambi mbali mbali.
g)
Kuendeleza ujenzi wa Hospital ya KMKM
Kibweni.
16.
Mheshimiwa
Spika, ili Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo
(KMKM) kiweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi, kwa mwaka wa fedha
2012/2013, naliomba Baraza lako Tukufu liidhinishe TZS 9,660 milioni kwa matumizi ya kazi za kawaida na TZS
200 kwa matumizi ya kazi za maendeleo.
JESHI LA
KUJENGA UCHUMI (JKU)
17.
Mheshimiwa
Spika, Jeshi
la Kujenga Uchumi limeanzishwa kwa Sheria Namba 6 ya mwaka 2003 na lina jukumu
la kuwafunza vijana katika nyanja za uchumi, kilimo, viwanda vidogo vidogo,
uvuvi na mafunzo ya amali pamoja na kutoa huduma ya ulinzi kwa Taasisi za
Serikali. Vijana wa JKU hufunzwa kwa kufuata mfumo wa ujenzi wa Taifa ili
waweze kujiajiri wenyewe wakati wanapomaliza mafunzo yao.
18.
Mheshimiwa
Spika, Jeshi
la Kujenga Uchumi (JKU), kwa mwaka wa fedha 2011/2012 liliidhinishiwa TZS 4,668
milioni kwa matumizi ya kawaida na TZS 450 milioni kwa kazi za maendeleo. Hadi
kufikia mwezi Machi 2012, Jeshi la Kujenga Uchumi liliingiziwa TZS 4,431.7
milioni sawa na asilimia 94.9 ya matumizi ya kawaida na TZS 195.6 milioni sawa
na asilimia 43.5 ya makadirio ya matumizi ya kazi za maendeleo na kutekeleza
yafuatayo:-
a)
Jeshi la Kujenga Uchumi limekamilisha
uchoraji wa ramani ya ujenzi wa Skuli ya Sekondari pamoja na kukusanya vifaa
mbali mbali vya ujenzi wa msingi wa jengo la ghorofa moja.
b)
Wafanyakazi 25 wamepatiwa mafunzo
katika fani ya sheria, udaktari, uuguzi, ualimu, uhasibu, ufugaji nyuki, ushoni
na kompyuta.
c)
Mazao ya aina mbali mbali yamelimwa ikijumuisha
ekari 156 za mpunga, ekari 82 za mahindi na mtama, ekari 80 za muhogo, ekari 13 za kunde, ekari nne za viazi vitamu ekari 21 za bustani ya miti ya
matunda.
d)
Jeshi la Kujenga Uchumi limenunua
mashine moja ya kutotoa vifaranga “incubator” ili kurahisisha upatikanaji wa
vifaranga na kazi ya kuzalisha vifaranga tayari imeanza na inaonesha maendeleo
mazuri.
e)
Jeshi la Kujenga Uchumi limechimba
kisima kimoja cha maji na cha pili kipo katika hatua za mwisho ili kurahisisha
upatikanaji wa maji safi na salama katika Skuli ya Ufundi na Sekondari ya JKU
Mtoni.
f)
Baadhi ya zana za kufundishia
zimenunuliwa kwa ajili ya kuimarisha mafunzo kwa vitendo katika Skuli ya Ufundi
JKU Mtoni.
g)
Ujenzi wa nyumba ya pili ya wataalamu Bambi
umekamilika na kuanza ujenzi wa msingi nyumba ya tatu. Kuchimba kisima kimoja
kwa ajili ya kuongeza uwezo wa maji ya umwagiliaji kwenye ekari 28 za mboga mboga na ekari 5 za
alizeti ambazo zimelimwa.
h)
JKU imefanya mapitio ya uendeshaji wa
shamba la mboga mboga Bambi ili kuweza kuleta tija kama ilivyokusudiwa.
i)
Kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo
na Maliasili, JKU imelima ekari 15 za mbegu ya mahindi, ekari 40 za mbegu ya
mpunga aina ya Nerica, ekari 10 za mbegu ya mtama.
j)
Kwa kushirikana na Vikosi vyengine JKU
imeshiriki katika operasheni karafuu kisiwani Pemba katika msimu huu wa karafuu
uliomalizika.
k)
JKU kwa kushirikana na JKT, imeshiriki
katika maonesho ya Saba Saba na Nane Nane katika Mikoa ya Dar es salam,
Morogoro na Dodoma. Pia Jeshi la Kujenga
Uchumi kwa njia ya uwakala limeleta matrekta 14 kutoka SUMA JKT kwa ajili ya
kurahisisha upatikanaji wa matrekta nchini.
l)
Vituo vya afya vya JKU Saateni na Wawi
vimetoa huduma kwa Askari na Maafisa wa JKU pamoja na raia wa maeneo jirani. Kwa
mwaka 2011/2012, jumla ya wagonjwa 27,653 wamepatiwa huduma tofauti za matibabu.
m)
JKU imeshiriki katika michezo ikiwemo
mpira miguu, mpira wa pete, mpira wa kikapu, mpira wa mikono, riadha pamoja na
kutoa burudani kupitia vikundi vyake vya sanaa na utamaduni.
n)
Jeshi la Kujenga Uchumi limeweza
kufanya ukarabati mkubwa wa majengo mbali mbali ikiwemo jengo la Ofisi ya JKU
Upenja, nyumba moja ya kuishi wafanyakazi na ukarabati mabanda ya kuku katika
kambi ya JKU Upenja.
o)
Kuendeleza ujenzi wa nyumba ya Kamanda
wa JKU Pemba.
19.
Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2012/1013, Jeshi la Kujenga Uchumi limejipangia kutekeleza
malengo yafuatayo:-
a)
Kuwaendeleza kielimu watumishi wa JKU
katika fani na ngazi mbali mbali ili kuleta ufanisi katika kazi.
b)
Kuendelea kutoa mafunzo ya uzalendo
kwa vijana wa Zanzibar ili waweze kuitumikia nchi yao.
c)
Kuimarisha ufugaji wa kuku na ng`ombe
wa maziwa pamoja na kufufua ufugaji wa nyuki.
d)
Kuimarisha kilimo cha mazao ya nafaka
na miti ya matunda
e)
Kuimarisha Skuli za Ufundi na
Sekondari za JKU kwa kuzipatia vifaa vya kufundishia mafunzo kwa vitendo ili
ziweze kutoa elimu bora kwa vijana.
f)
Kuendelea kutoa elimu juu ya mapambano
dhidi ya ugonjwa wa ukimwi kwa wana JKU.
g)
Kuimarisha na kupanua mafunzo ya
kijeshi kwa watumishi wa JKU
h)
Kuendeleza Michezo mbali mbali na
utamaduni
i)
Kuendelea kutengeneza mazingira bora kwa
kuwapatia wafanyakazi zana na vifaa vya kisasa vya kufanyia kazi pamoja na kutoa
maslahi kwa wapiganaji.
j)
Kuendeleza uimarishaji wa miundombinu
ya mradi wa shamba la mboga mboga liliyoko JKU Bambi.
k)
Kujenga ghala la kisasa la kuhifadhia
mazao na ujenzi wa nyumba ya tatu ya wataalamu Bambi.
l)
Kununua samani na vifaa vya nyumbani,
pamoja na kusimamia utendaji wa shughuli za kila siku za shamba.
20.
Mheshimiwa
Spika, ili Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) liweze
kutekeleza malengo yake kwa ufanisi, kwa mwaka wa fedha 2012/2013, naliomba
Baraza lako Tukufu liidhinishe TZS 7,504
milioni kwa matumizi ya kazi za kawaida na TZS 300 milioni kwa ajili ya
kazi za maendeleo.
IDARA YA CHUO
CHA MAFUNZO (MF)
21.
Mheshimiwa
Spika, Idara
ya Chuo cha Mafunzo imeanzishwa kwa Sheria Namba 1 ya mwaka 1980 na ina jukumu
la kuwapokea, kuwalinda wanafunzi na mahabusu kwa lengo la kuwarekebisha tabia
na kuwapatia taaluma ili wawe raia wema. Pia Idara inashirikiana na Idara Maalum
za SMZ na vikosi vya ulinzi na usalama vya SMT katika kuimarisha ulinzi,
usalama, utulivu na amani.
22.
Mheshimiwa
Spika, Idara
ya Chuo cha Mafunzo (MF), kwa mwaka wa fedha 2011/2012 iliidhinishiwa TZS 3,938
milioni kwa kazi za kawaida na TZS 400 milioni kwa matumizi ya maendeleo. Hadi
kufikia mwezi Machi 2012, Kikosi kiliingiziwa TZS 3,307.6 milioni sawa na
asilimia 84.0 ya makadirio ya matumizi ya kawaida na TZS 315.6 milioni sawa na
asilimia 78.9 kwa matumizi ya kazi za maendeleo na kutekeleza yafuatayo:-
23.
Mheshimiwa
Spika,
kwa mwaka wa fedha 2011/2012 Chuo Cha Mafunzo kimepokea jumla ya wanafunzi 479.
Kati ya hao, wanafunzi 462 ni wanaume na wanafunzi 17 ni wanawake. Idadi hii
inaonesha kuongezeka kwa wanafunzi 17 waliopokelewa Chuoni hapo ikilinganishwa
na mwaka wa fedha 2010/2011 kama inavyoonekana katika Kiambatanisho Namba 11.
24.
Mheshimiwa
Spika, Chuo
Cha Mafunzo kimepokea jumla ya mahabusu 2,620, kati ya hao 2,510 ni wanaume na
110 ni Wanawake. Mahabusu 2,110 waliruhusiwa kwa dhamana na wengine kuachiliwa
kwa kuonekana hawana hatia na waliobakia wanaendelea kusubiri hatma ya kesi
zao. Makosa makubwa ya wanafunzi wanaoletwa chuoni ni kuua, wizi wa kutumia
silaha, wizi wa mazao, shambulio, kubaka na kuvunja nyumba na kuiba. Hakuna mtu
hata mmoja aliopo kizuizini kwa masuala ya kisiasa.
25.
Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2011/2012, Idara ya Chuo cha Mafunzo imetekeleza malengo
yafuatayo:-
a)
Imepima mashamba ya Hanyegwa Mchana na
Kambi ya Kinumoshi na eneo la ujenzi wa gereza jipya Hanyegwa mchana.
b)
Imefanya matengenezo ya kuezeka Chuo
cha Mafunzo cha Ubago.
c)
Imeendelea na ujenzi wa Bweni la
kulala Wanafunzi Kinumoshi kwa kuweka madirisha 4 mapya na hatua ya plasta
inaendelea.
d)
Vifaa vya kuezekea nyumba ya familia
mbili Kangagani Pemba vimenunuliwa.
e)
Wanafunzi wote wamebadilishiwa kivazi
kwa kushonewa sare za rangi ya machungwa.
f)
Imeimarisha huduma za chakula kwa
wanafunzi na wanapata chakula cha kutosha kwa siku.
g)
Imelima Ekari 50 za mpunga, Ekari 100
za muhogo, Ekari 5 za Viazi vitamu na Ekari 25 za Mahindi katika mashamba yake
ya Kengeja, Kangagani, Ubago, Tungamaa, Kinumoshi na Langoni.
h)
Imepitia Sera ya Idara na kutayarisha
Mpango Mkakati kwa hatua ya awali.
i)
Mradi wa ujenzi wa Chuo kipya Cha
Mafunzo umeshaanza kwa kusafisha eneo la ujenzi, kununua vifaa vya ujenzi ikiwa
ni pamoja na mashine za kufyatulia matofali, dampa moja na kusogeza miundombinu
karibu na eneo la ujenzi kama vile maji na umeme.
26.
Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2012/2013, Idara ya Chuo cha Mafunzo Kimekusudia kutekeleza
malengo yafuatayo:-
a)
Kuendelea kuyapima na kuyapatia hati
miliki mashamba ya Chuo cha Mafunzo Ubago, Kengeja, Langoni, Tungamaa na
Kangagani.
b)
Kuendelea na ujenzi wa Chuo cha
Mafunzo cha Ubago, Bweni la Wanafunzi Kinumoshi na Bweni la Wanafunzi Kengeja.
c)
Kuanza Ujenzi wa Ofisi Kuu ya Chuo Cha
Mafunzo Pemba na kuendelea na ujenzi wa Ofisi ya Zoni ya Mashamba Unguja.
d)
Kulima Ekari 50 za mpunga, Ekari 130
za muhogo, Ekari 3 mbaazi, Ekari 55 za mahindi na Ekari 3 za kilimo cha
mbogamboga na kuendeleza kilimo cha Mikarafuu katika mashamba yake ya Kengeja,
Kangagani, Ubago, Tungamaa, Kinumoshi, Langoni na Hanyengwa Mchana.
e)
Kuweka vyoo katika Mabweni ya kulala Wanafunzi
katika Chuo cha Mafunzo cha Langoni.
f)
Kuanza ujenzi wa majengo ya Chuo kipya
cha Mafunzo Hanyegwa Mchana.
g)
Kukamilisha Mpango Mkakati wa Idara ya
Chuo cha Mafunzo.
27.
Mheshimiwa
Spika, ili
Idara ya Chuo cha Mafunzo (MF) iweze kutekeleza malengo yake kwa ufanisi, kwa
mwaka wa fedha 2012/2013, naliomba Baraza lako Tukufu liidhinishe TZS 5,890 milioni
kwa matumizi ya kazi za kawaida na TZS 400 milioni kwa ajili ya kazi za maendeleo.
KIKOSI
CHA ZIMAMOTO NA UOKOZI ZANZIBAR
(KZU)
28.
Mheshimiwa
Spika, Kikosi
cha Zimamoto na Uokozi kimeanzishwa kwa Sheria Namba 7 ya mwaka 99 na kina
jukumu la kusimamia shughuli zote za uzimaji moto na uokozi wa maisha na mali
za watu. Vile vile kikosi kina jukumu la kutoa huduma za zimamoto kwenye
viwanja vya ndege vya Unguja na Pemba. Aidha, Kikosi kinatoa ushauri wa kujinga
na moto kwa wananchi, Taasisi za Serikali na za watu binafsi.
29.
Mheshimiwa
Spika, Kikosi
cha Zimamoto na Uokozi (KZU), kwa mwaka wa fedha 2011/2012 kiliidhinishiwa TZS
1,883 milioni kwa kazi za kawaida na hadi kufikia mwezi Machi 2012, Kikosi kiliingiziwa
TZS 1,869 milioni sawa na asilimia 99.3 ya makadirio ya matumizi ya kawaida na
kutekeleza yafuatayo:-
a)
Kikosi kimenunua gari mbili za kisasa
za kuzimia moto na gari moja limepelekwa Pemba. Vile vile, vifaa vya aina mbali
mbali vimepatikana kwa upande wa Unguja na Pemba.
b)
Mawasiliano ndani ya Kikosi
yameimarika kwa kununua redio mpya 4, kufanyia matengenezo mbali mbali ya redio
zilizopo Kikosini na Uwanja wa Ndege.
c)
Kikosi kimesafisha na kuchimba msingi
kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mapumziko Chanjaani Pemba.
d)
Kikosi kimejenga banda la kuweka gari
za kuzimia moto katika Kituo cha Mwanakwerekwe.
e)
Kikosi kimejenga nyumba ya vyumba
vinne katika kituo cha Kigunda na kutia sakafu, plasta na sehemu ya mapokezi
imewekwa dari.
f)
Kikosi kimenunua mabati kwa ajili
kuezekea Kituo cha Zimamoto Kitogani.
g)
Kikosi kimejenga hodhi la kuhifadhia maji
katika kituo cha Chanjaani.
h)
Kikosi kinaendelea na ujenzi wa uzio
wa Kituo cha Mahonda.
i)
Kikosi kimenunua vifaa na samani kwa vituo
vyake vya Unguja na Pemba.
j)
Kikosi kimewapatia Maofisa na Askari sare
na vifaa vya kazi.
k)
Maafisa watatu wamehudhuria mafunzo
nchini Singapore, maafisa 6 fani ya uhasibu, 11 mafunzo ufundi, watatu shahada
ya sheria, wanne fani ya uboharia na manunuzi, 30 mafunzo ya uongozi mkubwa na
35 mafunzo ya uongozi mdogo
l)
Elimu imetolewa kwa njia ya redio na
TV ambapo jumla ya vipindi 36 vilirushwa hewani. Aidha, vipeperushi juu ya
kujikinga na majanga ya moto vimetengenezwa na maonesho ya utumiaji wa kifaa
cha kuzimia moto kinachoitwa “Dry Sprinkler Power Aerosal” (DSPA) yamefanyika
kwa Taasisi mbali mbali za binafsi na Serikali.
30.
Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2012/2013, Kikosi kimekusudia kutekeleza malengo yafuatayo:-
a)
Kuendelea kununua vifaa na gari za kutoa
huduma za kuzima moto na uokozi.
b)
Kuimarisha mawasiliano ya uhakika
ndani ya Kikosi.
c)
Kundelea kufanya matengenezo ya
majengo na kujenga vituo vipya katika maeneo mapya.
d)
Kuboresha mazingira ya kazi na maslahi
ya wafanyakazi.
e)
Kuboresha huduma za kiutawala na
michezo.
f)
Kukuza uwezo wa kiutendaji kwa Maafisa
na wapiganaji kwa kuwapatia mafunzo ndani na nje ya nchi.
g)
Kuongeza uhusiano na mashirikiano ya
namna ya kukabiliana na majanga mbali mbali kitaifa na kimataifa
h)
Kukuza uwelewa kwa wananchi, Taasisi
za serikali, sekta binafsi, ili kuchukua hatua za tahadhari ya kujikinga na
majanga ya moto.
31.
Mheshimiwa
Spika, ili
Kikosi cha Zimamoto na Uokozi (KZU) kiweze kutekeleza malengo yake kwa ufanisi,
kwa mwaka wa fedha 2012/2013, naliomba Baraza lako Tukufu liidhinishe TZS 3,099
milioni kwa matumizi ya kazi za kawaida.
KIKOSI
CHA VALANTIA ZANZIBAR (KVZ)
32.
Mheshimiwa
Spika, Kikosi
cha Valantia kimeanzishwa kwa Sheria Namba 5 ya mwaka 2004 na kina majukumu ya
kutoa ulinzi kwa kushirikiana na Vikosi vya ulinzi na usalama vya SMT na SMZ,
kusaidia kulinda raia na mali zao, kutekeleza shughuli za kijeshi kwa wakati wa
dharura..
33.
Mheshimiwa
Spika, Kikosi
cha Valantia (KVZ), kwa mwaka wa fedha 2011/2012 kiliingiziwa TZS 2,452 milioni
kwa kazi za kawaida na TZS 100 kwa kazi za maendeleo. Hadi kufikia mwezi Machi
2012, Kikosi kiliingiziwa TZS 2,086.7 milioni sawa na asilimia 85.1 ya
makadirio ya matumizi ya kawaida na TZS 50 milioni sawa na asilimia 50 kwa matumizi
ya kazi za maendeleo na kutekeleza yafuatayo:-
a) Kikosi
kimeshiriki katika majukumu ya ulinzi na shughuli za uokozi kwa kushirikiana na
vikosi vya SMT na SMZ.
b) Kimewapatia
elimu wapiganaji wake 13 katika fani za udaktari, uhasibu, mawasiliano ya redio,
manunuzi na ugavi, utawala wa umma, TEKNOHAMA, utunzaji wa kumbukumbu, raslimali
watu na mafunzo ya ufundi ndani na nje ya Zanzibar.
c) Kikosi
kimewapatia elimu ya ushauri nasaha juu ya kujikinga na maambukizi mapya ya UKIMWI
wapiganaji wake wote Unguja na Pemba.
d) Kikosi
kimewapatia sare Wapiganaji wake kwa kushonewa sare 500 na nyengine zinaendelea
kushonwa katika kiwanda cha Ushoni cha Idara Maalumu za SMZ.
e) Kikosi
kimeendelea kuyafanyia matengenezo ya vibanda vitatu vya walinzi Makao Makuu
Mtoni, matengenezo ya Kambi ya Kisakasaka na matengenezo ya Kambi ya Pangatupu
kwa Unguja. Kwa upande wa Pemba Kikosi kimefanya matengenezo katika Kambi ya
Ndugukitu.
f)
Kikosi kimeyapatia hatimiliki maeneo mawili
(Kambi ya Mtoni na Kambi ya Micheweni) na maeneo yaliyobakia taratibu za
kupatiwa hatimiliki zinaendelea.
g) Kikosi
kimekamilisha ujenzi wa jengo la Makao Makuu na ujenzi wa ghala la kuhifadhia
vifaa uko katika hatua za mwisho.
34.
Mheshimiwa
Spika, pamoja
na kutimiza majukumu hayo iliyojipangia pia Kikosi cha Valantia Kwa kushirikana
na vikosi vyengine kimeweza kushiriki katika operasheni karafuu kisiwani Pemba
katika msimu huu wa karafuu uliomalizika hivi karibuni.
35.
Mheshimiwa
Spika, kwa
mwaka wa fedha 2012/2013 Kikosi cha Valantia kitatekeleza malengo yafuatayo:-
a)
Kuimarisha nguvu za ulinzi na usalama.
b)
Kuwaongezea uwezo wa kiutendaji kwa
kuwapatia elimu Wapiganaji kwa kozi mbalimbali ndani na nje ya kikosi.
c)
Kuweka mazingira mazuri ya kazi
ikiwemo ununuzi wa gari.
d)
Kuendelea kuwapatia sare na vifaa vya
ulinzi wapiganaji wote wa Kikosi.
e)
Kutengeneza majengo ya kikosi na kuendelea
kuyapatia hatimiliki maeneo ya kikosi Unguja na Pemba.
f)
Kuendeleza ujenzi wa jengo la Makao
Makuu yakiwemo ujenzi wa mesi na ujenzi wa ukumbi wa mkutano.
36.
Mheshimiwa
Spika, ili
Kikosi cha Valantia kiweze kutekeleza malengo yake kwa ufanisi, kwa mwaka wa
fedha 2012/2013, naliomba Baraza lako Tukufu liidhinishe TZS 3,784 milioni kwa
matumizi ya kazi za kawaida na TZS 100 milioni kwa matumizi ya kazi za
maendeleo.
JUMLA YA MATUMIZI YA OFISI YA RAIS NA
MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI KWA MWAKA WA FEDHA 2012/2013
37.
Mheshimiwa
Spika, baada
ya kutoa maelezo juu ya utekelezaji wa malengo ya Idara na Taasisi zote zilizo
chini ya Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
sasa kwa ruhusa yako naomba kutoa maelezo ya muhutasari wa maombi ya fedha kwa
mwaka 2011/2012 na jumla ya matumizi hadi kufikia Machi 2012 na maombi ya fedha
kwa mwaka 2012/2013.
38.
Mheshimiwa
Spika,
kwa mwaka wa fedha unaoishia Juni 2012, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi, ilikadiriwa kutumia TZS 34,176.5 milioni. Kati ya hizo TZS 30,435.5
milioni kwa kazi za kawaida, TZS 1,930 milioni kwa kazi za maendeleo na TZS 1,811.0
milioni kwa ajili ya ruzuku za Baraza la Manispaa na Mabaraza ya Miji ya
Mkoani, Chake Chake na Wete. Hadi kufikia Machi 2012, Ofisi imeingiziwa TZS 26,570.8 milioni sawa na asilimia 87.3 kwa
kazi za kawaida, TZS 1,477.3 milioni sawa na asilimia 76.6 kwa kazi za maendeleo
na TZS 1,381.7 milioni sawa na asilimia 76.3 za ruzuku.
39.
Mheshimiwa
Spika,
ili Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
iweze kutekeleza malengo na majukumu yake kwa ufanisi, kwa mwaka wa fedha
2012/2013, inaomba kuidhinishiwa jumla ya TZS 50,698.1 milioni. Kati ya hizo,
TZS 46,654.1 milioni kwa ajili ya matumizi ya kazi za kawaida, TZS 1,906.0
milioni kwa matumizi ya kazi za maendeleo na TZS 2,138 milioni ni ruzuku kwa Baraza
la Manispaa na Mabaraza ya Miji (Mabaraza ya Miji ya Mkoani, Chake Chake na
Wete).
40.
Mheshimiwa
Spika, maelezo
ya uchambuzi wa kina wa fedha zilizoombwa kwa mwaka 2011/2012, fedha
zilizopatikana hadi mwezi Machi 2012, asilimia ya fedha zilizopatikana hadi
mwezi Machi 2012 na makisio ya bajeti kwa mwaka 2012/2013 kwa kila Idara
zimeoneshwa katika Viambatanisho Namba 12, 13 na 14. Aidha, Kiambatanisho Namba
15 kinatoa uchambuzi wa makushanyo ya fedha kutoka katika vyanzo vyao vya
mapato ya Baraza la Manispaa, Mabaraza ya Miji ya Mkoani, Chake Chake na Wete
na Halmashauri 9 za Wilaya.
HITIMISHO
41.
Mheshimiwa
Spika,
kwa kumalizia hotuba hii, naomba kuchukua fursa nyengine kumpongeza Mheshimiwa
Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
kwa uongozi wake makini wa kusimamia Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi na kuendelea kunipa dhamana ya kuiongoza Ofisi hii. Aidha, natoa
shukrani zangu za dhati kwa wananchi wa Zanzibar kwa kuendeleza hali ya amani
na utulivu iliyopo, kabisa tusiichezee. Natoa wito kwa wananchi kuendelea
kuheshimu Sheria za nchi tulizoziweka wenyewe kwa lengo la kujenga mustakbali
mwema wa maendeleo ya nchi yetu.
42.
Mheshimiwa
Spika,
mwisho, nawashukuru viongozi, watendaji na wafanyakazi wote wa Ofisi ya Rais na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa ushirikiano wao wa karibu wanaoendelea
kunipa kila siku katika kutekeleza kazi zetu. Nawashukuru wote kwa kunisikiliza
kwa makini wakati wote na natanguliza shukrani zangu kwa Waheshimiwa Wajumbe wa
Baraza hili Tukufu kwa michango mtakayoitoa katika kujadili hotuba ya bajeti
hii.
43.
Mheshimiwa
Spika,
naomba kutoa hoja.
(Dkt.
Mwinyihaji Makame)
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
Zanzibar.
No comments:
Post a Comment