Hafsa Golo na Gilbert Massawe
WIZARA ya Afya imesema serikali itahakikisha
wanatoa huduma za kina mama wajawazito na kujifunguwa zinatolewa bila ya malipo
ili kuondosha vikwazo ambavyo vinaweza kujitokeza na kuwahatayarishia maisha
kinamama kwa kutomudu fedha za kununulia vifaa.
Naibu wa wizara ya Afya Dk. Sira Ubwa Mwamboya
alisema hayo katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi wakati alipokuwa akijibu
suala lililoulizwa na Mwakilishi wa jimbo la Muyuni, Jaku Hashim Ayoub aliyetaka
kujua hatua zilizochukuliwa na wizara katika kuhakikisha akinamama wanajifungua katika hospitali za serikali wanapata huduma hizo bure kama alivyoagizwa Rais.
Alisema kuwa serikali kupitia bajeti ya
wizara ya afya ya mwaka 2012/2013 itaiongezea fedha ili kuweza kukidhi mahitaji
ya huduma hizo za akina mama.
Sambamba na hayo, alisema hatua ambazo
serikali imezichukuwa ni kuwaruhusu
kutiliana mkataba wa muda mrefu na wanunuzi na wasambazaji wa dawa waliopata
tenda.
Alisema kuwa pamoja na mpango wa huduma za
kinamama na watoto utachangia vifaa muhimu kwa ajili ya kuisaidia kutekeleza
agizo hilo.
Akijibu la nyongeza lililoulizwa na Mwakilishi
wa jimbo la Muyuni na Jaku Hashim ambaye alitaka kujua wizara inampango gani
wakuongeza madaktari ili kuondoa kilio mama wajawazito.
Alisema kuwa suali hilo halina njia ya kuweza kufanyika kwani
wanawake wenyewe hawana hamu ya kusomea fani hiyo, ndio maana madaktari wengi
wa maradhi ya wanawake ni wanaume.
“Suala la maradhi ya kike la kuongeza madaktari
wanawake kuchukuwa fani ya utaalamu wa maradhi ya kike (gynecologist) halina
uhusiano wa moja kwa moja kwa sababu hii ni hiyari na maamuzi ya daktari
mwenyewe”,alisema.
Hivyo alisema katika kutatua tatizo hilo ni vyema kujipanga
upya na kuwahimiza watoto kosoma masomo ya sayansi na kuwashawishi wasomee
udaktari wa wanawake.
No comments:
Post a Comment