Habari za Punde

Zanzibar kutekeleza maazimio ya Rio+20


Na Salum Vuai, MAELEZO
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar, inajipanga kuhakikisha inatekeleza maazimio yaliyopitishwa katika mkutano wa maendeleo endelevu (Rio+20), uliofanyika jijini Rio de Janeiro, Brazil Juni 20 hadi 22 mwaka huu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Fatma Abdulhabib Ferej aliyekuwemo kwenye ujumbe wa Tanzania, alisema miongoni mwa mikakati hiyo, ni pamoja na kuimarisha utekelezaji wa mipango iliyopo.

Akizungumzia malengo ya katika mkutano huo uliojumuisha marais, viongozi wa serikali na mashirika ya kimataifa waziri huyo alisema mafanikio katika utekelezaji wa maazimio ya Rio ya mwaka 1992 yatafanyiwa tathmini na kutambua mapungufu yaliyojitokeza katika utekelezaji wake.


Alisema ni kupata ridhaa ya kisiasa ya kuendelea kuimarisha utekelezaji wa maazimio ya mwaka 1992, na kutambua changamoto zinazokwamisha utekelezaji wake na kupanga hatua za baadae.

Aidha, mkutano huo umebaini kuwa, dunia imeshuhudia kukosekana kwa uhakika wa chakula, njaa, upungufu wa maji, kuongezeka kwa umasikini, ukataji ovyo wa miti, matatizo mbalimbali ya kijamii, ukosefu wa ajira na kuanguka kwa uchumi wa dunia.

Hata hivyo, Ferej alisema pamoja na changamoto hizo, Tanzania ilishiriki mkutano huo ikiwa imepata mafanikio mbalimbali katika utekelezaji wa azimio la Rio la mwaka 1992, ikiwemo uundwaji wa taasisi tafauti, sera na sheria zinazosimamia shughuli za mazingira.

Alitoa mfano kwa upande wa Zanzibar kuanzishwa kwa Idara ya Mazingira mwaka 1989 kabla ya azimio la Rio 1992, ambapo imemudu kuanzisha sera ya mazingira ya 1992 na sheria ya mazingira ya mwaka 1996, kutayarishwa kwa dira ya maendeleo 2020, mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umasikini (Mkuza     I na II-2000/05 na 2010/2015).

Alifafanua kuwa malengo hayo yanaelekea zaidi katika azma ya kuongeza ajira, matumizi endelevu ya rasilimali za bahari na maandalizi makini ya kukabiliana na majanga, mafuriko na ukame.

Waziri huyo alisema mipango ya Zanzibar katika kutekeleza maazimio hayo, ni kuimarisha uwezeshaji wa sekta mbalimbali pamoja na wananchi, ukuaji wa teknolojia, upatikanaji wa vitendea kazi na fedha.

Aidha alieleza kuwa, serikali itaendelea kuimarisha uhusiano mzuri uliopo na wadau wa maendeleo na mashirika ya kimataifa ikiwemo UNDP, UNEP, FAO na mengineyo katika kutafuta vyanzo mbalimbali vya rasilimali zitakazosaidia kuimarisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Aliahidi kuwa, serikali itaimarisha usimamizi wa rasilimali zitakazotumika wakati wa utekelezaji wa maamuzi ya mkutano huo ili kuhakikisha uthamani wa fedha zinazotolewa na washirika wa maendeleo ili kuongeza imani kwa washirika hao na wananc

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.