Na Hafsa Golo
Kutokana na hali
iliyojitokeza, kuna uwezekano mkubwa zana na vifaa vilivyowekwa kwa mradi huo
kuharibika kutokana na muda pamoja na kukosa utunzaji wa kitaalamu.
Waziri huyo
alisema wizara yake haina sababu ya kutoingilia suala hilo kwani kumalizika kwa
kituo hicho kutawapa fursa wakulima na wajasiriamali kuzalisha bidhaa zenye
kiwango na kuweza kusarifu matunda kwa njia tofauti kutokana na wingi wa mazao
yaliyopo eneo hilo na Zanzibar kwa jumla ili kuepuka wakulima kupoteza nguvu, bila mafanikio.
Waziri Mazrui
alisema kuwepo kwa Kituo cha Usarifu wa Mazao Zanzibar ni muhimi kwani
kitawezesha kusaidia vijana kupata ajira huku wakulima na wajasiriamali
wakijiandaa kupata mafunzo na wakulima kupata soko kwa mazao yao.
Aidha alisema
lengo la kiwanda hicho pamoja na kusarifu matunza lakini pia kingetumika kutoa
mafunzo kwa wajasiriamali, mbali mbali na pia kingetumika kulisarifu zao la
muhogo na matunda mengine ili kuvutia watalii wanaolitembele eneo hilo kila
siku.
Hata hivyo,
alisema pamoja na changamoto iliyojitokeza lakini jambo la msingi ni
kuhakikisha malengo yaliyokusudiwa yaweze kufikiwa tena kwa wakati unaofaa.
"Hili ni
jambo zuri kwani wajasiriamali na wakulima watapata ujuzi na wataweza kupewa
mafunzo watu wengi kwani taasisi hii ingetoa msukumo wa ajira pia itashajiisha
wakulima kuwa na ari ya kuzalisha mazao bora," alisema.
Kwa mujibu wa
taarifa ya Mratibu wa usarifu wa mazao Kizimbani, Saleh Muhammed Juma, alisema sababu kuu ya kusita mradi huo,
ni Mkandarasi wa mradi huo kubeba majukumu mengine ya ujenzi, huko Morogoro,
hali inayodaiwa kusababisha ujenzi huo kusuasua kwa muda mrefu hadi kufikia
kukatishwa mkataba.
Alisema Mradi
huo kwa jumla uliofadhiliwa na KOICA uligharimu dola milioni 2.3 za Marekani, ambapo
ujenzi wa kituo ulitengewa dola 450,000.
Aidha alisema
kuwa mradi huo pia umewasilisha vifaa mbali mbali vikiwemo mashine za kusagia
matunda, vifaa vya maabara na mashine za kusagia uwanga.
Pia alimuomba
Waziri huyo kuhakikisha jitihada zinachukuliwa kukamilisha mradi huo ili
kuihamasisha jamii kukitumia kituo hicho kujifunza utengenezaji bidhaa mbali
mbali za matunda na viungo.
Naye Mkururugezi
uendeshaji na utumishi, Wizara ya Kilimo, Asha Ali Juma, alisema kuwa ni vyema
serikali kwa kushirikiana na wizara hizo mbili kutafuta mbinu mbadala ili kituo
hicho kimalizike kwa wakati ili vifaa vilivyopo viweze kutumika kabla
havijamaliza muda.
No comments:
Post a Comment