MKUTANO WA 36
WA “ADIMINISTRATIVE COUNCIL” YA ARIPO
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mkutano
wa 36 wa Baraza la Utawala la ARIPO (ARIPO Adiministrative Council),
unaondaliwa kupitia Afisi ya Mrajis Mkuu wa Serikali na Mamlaka ya Usajili wa
Biashara na Leseni (BRELA) kwa kushirikiana na Shirika la kusimamia Mali za
Ununifu la Kanda ya Afrika (African Regional Intellectual Property Organization
–ARIPO).
Mkutano huo wa kimataifa utachukua muda wa siku tano kuanzia tarehe 26 –
30 Novemba 2012, utafanywa katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli Zanzibar Beach
Resort iliyoko Mazizini nje kidogo ya mji wa Zanzibar, ambapo Mgeni Rasmi
atakaefungua Mkutano huo anatarajiwa kuwa Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar,
Maalim Seif Sharrif Hamad.
Jumla ya washiriki 75 kutoka nchi wanachama wa ARIPO pamoja na waalikwa
kutoka nchi za Afrika na nje ya Afrika, pamoja na wawakilishi wa Mashirika
mbalimbali yanayosimamia mali za ubunifu wanatarajiwa kushiriki katika mkutano huo.
Shirika hili (ARIPO) limeanzishwa mjini Lusaka, Zambia, terehe 9 Disemba, 1979 kupitia
mkataba maalum unaojulikana kama Makubaliano ya Lusaka (Lusaka Agreement), kwa
lengo la kuimarisha mashirikiano katika kulinda
rasilimali za nchi wanachama, kushirikiana, kubadilishana taarifa pamoja na kuweka misingi ya pamoja ya sheria
katika kusimamia kazi za Tasnia ya Mali za Ubunifu (zikiwemo Alama za biashara
(TradeMark), Hataza /uvumbuzi (Patent), miundo (Design), Viashiria vya mahala
(Geographical Indications), Hakimiliki (copy rights) katika kila nchi
mwanachama wa shirika hili.
Madhumuni makuu ya ARIPO yamebainishwa katika kifungu cha tatu cha
Mkataba wa Lusaka, ambayo ni pamoja na kuweka misingi ya kushirikiana kwa
madhumuni ya kufikia maendeleo ya teknolojia na kiuchumi kwa nchi
wanachama kuimarisha usimamizi wa Tasnia
za Mali za Ubunifu.
ARIPO inaundwa na vyombo viwili vikuu ambavyo ni Baraza la Mawaziri (Council of Ministers) ambalo wajumbe
wake ni Mawaziri wanaosimamia Mali za Ubunifu katika nchi wanachama na Baraza
la Utawala (Administrative Council) ambalo wajumbe wake ni wakuu wa taasisi au
idara zinazosimamia Mali za Ubunifu katika nchi wanachama. Makao
makuu ya shirika hilo yapo Harare, Zimbabwe.
Baraza la Utawala
linakutana kila mwaka katika chini mwanachama itayoomba na kukubaliwa kuandaa
mikutano hiyo. ARIPO ina jumla ya nchi wanachama kumi na nane
(18) ambazo zinazozungumza lugha ya Kiingereza ambazo ni wanachama wa shirika
hilo ni pamoja na Botswana, the Gambia, Ghana, Kenya, Lesotho, Malawi, Mozambique, Namibia,
Sierra Leone, Liberia, Rwanda, Somalia, Sudan, Swaziland, Tanzania, Uganda, Zambia na Zimbabwe.
Miongoni mwa faida zilizopatikana na nchi wanachama
kutokana na ARIPOni kuziweka pamoja rasilimali watu na rasilimali fedha,
ambapo nchi nchi wanachama zimeweza
kufaidika kimaendeleo na kiuchumi kutokana na kupata fursa ya kutumia
rasilimali adimu mbazo na muhimu kwa mahitaji na maendeleo ya nchi wanachama na raiya wake.
Umuhimu wa kusimamia
rasilimali hizi zinazotokana na mali za ubunifu, umedhihihirika katika nchi
mbalimbali ambazo zimetoa kipaumbile katika kusimamia mali za ubunifu. Mfano
mzuri wan chi zilizofaidika kwa kusimamia vizuri mali za ubunifu ni Korea ya
Kusini. Kipindi kifupi kilichopita Korea ya Kusini ilikuwa mingoni mwa nchi
masikini duniani kutokana na kukosa rasilimali za asili zenye ubora. Kwa sababu
nchi hii imeweka mikakati imara ya kusimamia mali za ubunifu imeweza kupiga
hatua kubwa za kimaendelea tena kwa haraka, na kuiweka katika nafasi ya nne
katika nchi zilizoendelea kwa teknolojia ambapo ya kwanza ni Marekani
inayoifuatiwa na Japani na China.
Hii ni mara ya kwanza kwa Zanzibar kuwa mwenyeji wa mkutano huu, lakini
ni mara ua pili kwa Tanzania. Mkutano wa kwanza ulifanyika jijini Dar es
Salaam. Miongoni mwa mambo yatakayojadiliwa katika Mkutano huu wa 36 ni pamooja
na Bajet ya kuendeshea shughuli za ARIPO, Masuala ya utendaji na uwajibikaji,
Taarifa za utekelezaji za nchi wanachama, semina kuhusu Teknolojia ya Habari na
viashiri vya pahala (geographical Indication) na uchaguzi wa viongozi wapya wa
ARIPO. Aidha washiki watapata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya
kihistoria.
Serikali inatoa wito kwa vyombo vyote vya habari nchini kutoa taarifa
kwa wananchi juu ya umuhimu wa mkutano huu na usimamizi wa mali za ubunifu.
Mali za ubunifu ni moja kati ya nyenzo muhimu katika kuimarisha uchumi na
kuleta maendeleo ya nchi katika sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na teknolojia,
kilimo, sanaa na utamaduni. Aidha waandishi wa habari wanaomba wafuatilie
mwenendo wa mkutano huo ili waweze kuwaarifu wananchi juu ya mambo mbalimbali
yatayojadiliwa katika mkutano huo. Halikadhalika Serikali inawaomba wananchi
watoe ushirikiano kwa watendaji wake pamoja na wageni watakaoshiriki katika mkutano huo.
Imetolewa na:
Afisi ya Mrajis Mkuu wa Serikali
Zanzibar,
Na
Wakala wa Usajili wa Biashara na
Leseni
Tanzania.
No comments:
Post a Comment