Na Fatuma Kitima,DSM
JUKWAA
la Katiba Tanzania
(JUKITA) limesema katika muongozo wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba juu ya muundo
na utaratibu wa kupata wajumbe wa mabaraza ya katiba ya wilaya na asasi una
mapungufu katika baadhi ya vipengele.
Akizungumza
Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania, Deus Kibamba alitaja
baadhi ya mapungufu hayo kuwa Madiwani wasiwe wajumbe wa moja kwa moja wa
mabaraza ya katiba ya Wilaya,maoni juu
ya mwongozo yametolewa na watu wachache,sifa za watakaochaguliwa kuwa wajumbe
wa mabaraza ya katiba ya wilaya pia zina mapungufu.
Deus
alisema ili kupanua wigo wa demokrasia na kuepuka mgongano wa kimaslahi, Jukwaa
limependekeza kuwa Madiwani wasiei wajumbe wa moja kwa moja kwa nyadhifa
zao,katika mabaraza ya Wilaya ,ngazi ya serikali za mitaa na badala yake
wanaotaka kuwa wajumbe waombe ridhaa
mpya ya wananchi ili kuweza kuchaguliwa katika mabaraza hayo.
Alisema
sababu za kutoa mapendekezo hayo kuwa Madiwani wasingie kwa nafasi zao kwa
sababu Madiwani walichaguliwa kwa ajili ya kazi ya kuwawakilisha wananchi
katika ngazi ya mabaraza ya Madiwani ya Wilaya,manispaa,miji na majiji na si
kwa ajili ya mabaraza ya katiba.
Alieleza
wawakilishi wanne watakaochaguliwa kutoka kila kijiji na kata watakuwa na
mamlaka stahili ya kuwakilisha wananchi kama
ilivyo kwa Madiwani katika mabaraza ya Madiwani.
Alifafanua
kuwa uwakilishi wa Madiwani utaleta mgongano wa itikadi za vyama vilivyowaweka
Madiwani hao madarakani hivyo kuleta msuguano kwenye mchakato wa mabaraza ya
katiba.
Aidha
alisema kuingia kwao moja kwa moja kutaweka mazoea mabaya kwa vyombo
vitavyoundwa siku za baadae katika mchakato huo wa katiba pamoja na kuleta
utata juu ya endapo Wabunge ambao nao ni
wajumbe kwa nyadhifa zao.
Sababu
nyingine kuwa Madiwani jukumu lao ni usimamamizi wa shughuli za maendeleo na
masuala ya uongozi na siasa katika kila kata hivyo wanashauriwa Madiwani wabaki
hivyo ili wasaidie wanapohitajika katika majukumu hayo ya kila siku kuliko
wakiwa wajumbe katika mabaraza ya katiba.
Alisema
walibaini kuwa muongozo unatoa madaraka yasiyo na ukomo kwa watendaji wa vijiji
na masheha katika kuratibu zoezi la upatikanaji wa wajumbe wa mabaraza ya
katiba.
Alisema
Pamoja na mapendekezo hayo, muongozo utamke bayana namna madaraka hayo
yanavyodhibitiwa kwa kutamka watu wanaoweza kumzuia asiweke upendeleo kwa
baadhi ya watu waliopendekezwa kuwa wajumbe wa mabaraza ya katiba.
Hata
hivyo, alisema endapo mapungufu yatafanyiwa kazi muongozo huo utakuwa ni mfano
wa kuigwa na utafanya kazi ya mabaraza ya katiba yawe ya wazi na shirikishi kwa
kiwango kikubwa.
No comments:
Post a Comment