Mtume Muhammad Swalla
Allaahu ‘Alayhi Wasallam amesema:
( من ترك ثلاث جمع تهاونا طبع الله على قلبه )
Mwenye kuacha kusali Sala
tatu za Ijumaa kwa mpigo kwa kutojali (na kutoona umuhimu wake) Allaah atampiga
muhuri kwenye moyo wake. Muslim
Sala ya Ijumaa si jambo la
khiari kwa Muislamu bali ni fardhi ya lazima
( Fardhu ‘Ayn).
Si sahihi kwa Muislamu kutoonesha umuhimu katika jambo Allaah Subhaanahu Wata’ala amelipa umuhimu mpaka kuamua kuupiga muhuri moyo wa mja wake abakie miongoni mwa walio katika mghafala na kughafilika wakati kila siku tunarudi kwa Mola wetu na kumuomba ‘Ewe mwenye kubadlisha nyoyo zithibitishe nyoyo zetu katika kukutii Wewe’ Iweje nyoyo zetu zipigwe muhuri na Allaah kwa sababu ya kudharua maamrisho yake?.
( Fardhu ‘Ayn).
Si sahihi kwa Muislamu kutoonesha umuhimu katika jambo Allaah Subhaanahu Wata’ala amelipa umuhimu mpaka kuamua kuupiga muhuri moyo wa mja wake abakie miongoni mwa walio katika mghafala na kughafilika wakati kila siku tunarudi kwa Mola wetu na kumuomba ‘Ewe mwenye kubadlisha nyoyo zithibitishe nyoyo zetu katika kukutii Wewe’ Iweje nyoyo zetu zipigwe muhuri na Allaah kwa sababu ya kudharua maamrisho yake?.
Tuamke ndugu zangu katika
imani na kujihimu kuitekeleza Sala ya Ijumaa kila wiki kadri ya Allaah
Subhaanahu Wata’ala alivyotuwezesha kwa kutujaalia neema zake za siha, afya, uzima
na uwezo wa kuitekeleza ibada hii muhimu.
No comments:
Post a Comment