Na
Hassan Hamad, OMKR
WAZAZI
na walezi wameaswa kuacha tabia ya kuwaogopa watoto wao na badala yake
wawaongoze katika malezi yenye kufuata maadili mema.
Wito
huo umetolewa na mke wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, mama Awena Sinani
Massoud, wakati akizungumza katika hafla ya maulid ya kuzaliwa Mtume Muhammad
(SAW), yaliyoandaliwa na Madrasat Azhar ya Tomondo kiziwa maboga.
Alisema
tabia iliyozuka kwa baadhi ya wazazi kuogopa kuwakanya watoto wao ni hatari na
inapaswa kupigwa vita.
Aidha
aliwaomba wazazi kufuatilia maendeleo ya watoto wao katika madrasa, ili kubaini
iwapo wanafahamu ipasavyo au wanahitaji nguvu ya ziada katika kuwasomesha.
Aliwakumbusha
wazazi kuwazoesha watoto kuwa na subra na kutosheka na kile wanachopata kwa
mujibu wa uwezo wa wazazi au familia zao.
Alisema
iwapo utamaduni huo utaendelezwa, vijana wengi watazoea hali ya maisha
waliyonayo na kuacha tamaa ya kuiga au
kutamani baadhi ya vitu wasivyokuwa na uwezo navyo.
Aliwahimiza
waislamu kuendelea kuzinduana juu ya mambo ya kheri na yale yanayomchukiza
Mwenyezi Mungu, ili kulinda hadhi ya uislamu duniani.
Katika
risala yao kwa mgeni rasmi, walimu na wanafunzi wa madrasa hiyo walisema
wanakusudia kuanzisha skuli ya maandalizi ya kiislamu katika eneo hilo, lakini
bado wanakabiliwa na tatizo la eneo la kujenga skuli hiyo.
No comments:
Post a Comment