Na
Mwandishi wetu, MBEYA
MBUNGE
wa Mbeya Vijijini, Lackson Mwanjali (CCM) amejeruhiwa baada ya kushambuliwa na
watu wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Habari
zinasema, Mbunge huyo alishambuliwa pamoja na wenzake jana asubuhi katika
uchaguzi wa udiwani kata ya Santilya.
Mbunge
huyo na wenzake walishambuliwa baada ya kuzuka vurugu kati ya wafuasi wa CCM na
Chadema waliokuwa wamejazana katika vituo vya kupigia kura.
Hata
hivyo, vurugu hizo zilizimwa na polisi waliokuwa wakifanya doria kuhakikisha
uchaguzi huo unakuwa salama.
Watu
saba wanaoaminika kuwa wafuasi wa CHADEMA wanashikiliwa na polisi wakihusishwa
na tukio la kumshambulia Mbunge huyo.
Na
huko Bagamoyo gari nilalosadikiwa kuwa la CCM limekamatwa na wafuasi wa Chadema likidaiwa
kuwa na silaha za jadi yakiwemo mapanga na kuwashambulia watu waliokuwemo
pamoja na kuliharibu vibaya gari hilo .
Chama
cha Mapinduzi mkoani wa Pwani kimelaani vurugu hizo zilizotokea kata ya
Magomeni kikidai zilifanywa na wafuasi
wa CHADEMA na CUF.
Akizungumza
na waandishi wa habari ofisi za CCM wilaya hiyo, Katibu wa CCM mkoa wa Pwani,
Sauda Mpambalioto, alisema wafuasi hao mbali ya kuharibu na kuwapiga wafuasi wa
chama chao pia waliiba fedha na simu.
Alisema
gari lililoharibiwa lina namba za usajili T 112 BBF ambapo pia wafuasi hao wa
vyama vya upinzani walitumia silaha za jadi kuwajeruhi wafuasi wa CCM na
viongozi wao.
"Tunashangaa
ni kwanini wanafanya fujo kwani kila kitu kiko wazi kama waliona sisi tumekiuka
taratibu wangefuata sheria kuliko kufanya vurugu ambazo zimesababisha gari letu
kuvunjwa vioo na kuharibika vibaya,”alisema.
Kwa
upande wake moja ya viongozi wa CUF ambaye alijitambulisha kwa jina la Hassan
Kingwelu, alisema silaha hizo zilikuwa ndani ya gari la CCM kwa lengo la
kuvuruga uchaguzi.
Msimamizi
wa uchaguzi wa kata ya Magomeni, Mahafudh Jembe, alisema hadi wakati huo
alikuwa bado hajapokea taarifa yoyote kuhusu vurugu hizo.
Alisema
uchaguzi ulifanyika baada ya diwani wa kata hiyo, Jafar Yusuf, kufariki dunia.
Chaguzi
za udiwani zilifanya jana katika kata 27 za Tanzania Bara baada ya madiwani
wake kufariki dunia au kufukuzwa na vyama vyao.
kiukweli sumu zinazopandikizwa ndani ya mioyo ya baadh ya vijana itakuja kutugharimu.
ReplyDeleteMungu ikumbuke Tanzania kwni kila kukicha balaa tupu.
ReplyDelete