Na
Mwashamba Juma
MAGEUZI
katika uwajibikaji yanahitajika hasa katika sekta ya utalii Zanzibar ili kuwainua wazawa na changamoto ya
ajira.
Waziri
wa Habari, Utamaduni Utalii na Michezo, Mhe. Said Ali Mbarouk, alisema hayo
wakati akizungumza na wahitumu wa Chuo cha Maendeleo ya Utalii (ZIToD) katika
mahfali ya tano ya chuo hicho.
Alisema
wakati umefika kwa taasisi za utalii nchini kutoa kipaombele cha ajira kwa
wazawa badala ya nafasi kubwa kupewa wageni.
Alisema
Wazanzibari wana uwezo na kumudu nafasi hizo endapo watapatiwa taaluma na
uzoefu katika fani zao.
Aliwataka
wahitimu kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu kwa ambao watabahatika kuajiriwa
ili kuonesha uwezo kwa waajiri wao pamoja na kukabiliana na soko la ajira lenye
ushindani mkubwa.
“Ajira
sio lazima serikalini, bali hata kujiajiri mwenyewe kwa kuunda vikundi kutokana
na taaluma za fani zenu, tumieni ujuzi wenu kwa kuwa wabunifu ili mujiajiri na
kuajiri wengine,” alisema.
Alitumia
nafasi hiyo kupongeza juhudi za serikali kwa kukiweka chuo hicho kama sehemu ya Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) na kuongeza
kuwa bidiii zinahitajika kukuza fani ya utalii katika chuo hicho ili
kukabiliana na ushindani katika soko la ajira kwani fani ya utalii inasomwa
hadi ngazi ya shahada ya uzamivu (PhD).
Alisema
katika kuendana sambamba na mahitaji ya soko la ajira kwenye sekta hiyo chuo
kimeongeza majengo na fani mbalimbali, hasa katika masuala ya uongozi wa mahoteli na watembeza watalii.
Akitoa
mwelekeo wa maendeleo ya chuo, Mwenyekiti wa Baraza la chuo hicho, Khamis Mussa,
alisema sekta ya utalii ni moja ya sekta kiongozi katika uchumi wa Zanzibar na kuongeza kuwa
chuo kinajitahidi kutoa elimu yenye ubora ili kukabiliana na ushindani katika
soko la ajira duniani.
Alisema
katika kuongeza nguvu kwenye sekta ya utalii baraza lina mpango wa kuanzisha chuo
kama hicho katika visiwa vya Pemba ambacho
kitatoa wanafunzi wenye ubora ambao wataweza kushindana katika soko la ajira.
Aliahidi
kuzifanyia kazi changamoto zinazokikabili chuo hicho ikiwemo kuongeza kompyuta.
Kuhusu
changamoto ya mmong’onyoko wa ardhi katika maeneo karibu na fukwe za bahari
pamoja na tatizo la usafiri kwa wanafunzi chuoni hapo, alisema chuo
kinazifanyia kazi na kuadihi ndani ya kipindi kifupu matatizo hayo yataondoka.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa chuo hicho, Zulekha Kombo, alisema chuo kinajitahidi
kutafuta wafadhili kwa lengo la kujiboresha.
Nao
wa wanafuzi hao waliahidi kuzitumia taaluma zao kwa kutoa huduma zenye uobora katika
maeneo yao ya
kazi.
Jumla
ya wanafunzi 650 wa fani mbalimbali walitunukiwa vyeti.
No comments:
Post a Comment