Baadhi ya Washiriki wa Kongamano, la Kuchangia Mjadala wa Katiba uliofanyika katika Ukumbi wa Chjuo Kikuu cha Zanzibar SUZA na kuwashirikisha Wananchi mbalimbali na Wanasiasa na Viongozi wa Dini Zanzibar kujadili Rasimu ya Pili ya Katiba a
WAKATI
mkutano maalum wa bunge la katiba ukitarajiwa kuanza Februari 18, wajumbe
kutoka Zanzibar
wametakiwa kuweka mbele maslahi ya nchi badala ya vyama.
Aidha
wameonywa kwamba kama fursa hiyo
wataichezea watajuta maishani mwao
pamoja na kusababisha mashaka makubwa makubwa kwa vizazi vyao.
Wakichangia
mjadala wa katiba uliofanyika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) kampasi
ya Vuga, washiriki, walitahadharisha kwamba kama Zanzibar itazembea na kuweka
mbele maslahi ya vyama, matatizo yaliyopo sasa yatakuwa makubwa zaidi siku za
usoni na wakati huo hakutakuwa na mtu wa kuyasema kwa sababu fursa ilitolewa
ikachezewa.
Akifungua
mjadala huo, Jaji wa Mahakama Kuu Zanzibar, Mshibe Ali Bakar, aliwatoa hofu
wajumbe akisema wasihofu kuzungumza kwa sababu tu miongoni mwa wajumbe wamo
viongozi wa serikali na vyama vya siasa.
Alisema
katika bunge hilo
watu wote sawa bila kujali kiongozi au raia wa kawaida na kwamba wote wana haki
ya kuzunguza na kutoa michango inayojenga bila woga.
Hata
hivyo, alitahadharisha kwamba kama Wazanzibari hawaweka kando misimamo ya vyama
vyao, athari itakayoletwa na matokeo ya katiba mpya ni kubwa zaidi.
Mwakilishi wa wanawake, Asha Bakar Makame, alihimiza umoja na mshikamano miongoni mwa
wajumbe bila kujali itikadi.
Mwakilishi
wa Kwamtipura, Hamza Hassan Juma, alionesha hofu na sheria ya mabadiliko ya
katiba, akisisitiza umuhimu wa kuwepo usawa kati ya Zanzibar
na Tanganyika .
Mwakilishi
wa Magomeni, Salmin Awadh yeye alitilia wasi wasi uwezo wa Zanzibar kuchangia
serikali ya Muungano iwapo kutakuwa na mfumo wa serikali tatu, akisema Zanzibar haitakuwa na
uwezo wa kuchangia na kwamba hali hiyo inaweza kuvunja muungano.
Hata
hivyo, mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole, alisema
mapato ya serikali ya Muungano
yameanishwa ndani ya rasimu jinsi yanatavyopatika, akisisitiza kwamba
taasisi za fedha nchini (BoT, TRA na ZRB) zimethibitisha kwamba fedha hizo
zitapatikana.
Aidha
alisema Muungano umejengwa katika misingi mitatu muhimu ambayo ni usawa,
mshikamano na kusaidiana akisema nchi moja ikipata shida ni wajibu wa mshirika
wake kusaidia.
“Watanganyika
wakipata shida, rasimu imewawajibisha wenzao wa Zanzibar kuwasaidia kwa hali na
mali na hivyo hivyo iwapo Wazanzibari watapata shida,” alisema.
Mjadala
huo uliowashirikisha wasomi, wafanyabiashara, wanasiasa, wananchi, baadhi ya wajumbe wa bunge maalum
la katiba na Wawakilishi uliandaliwa na Taasisi ya Utafiti na Sera (ZIRPP) kwa
msaada wa Foundation for Civil Society.
No comments:
Post a Comment