Na Mwandishi wetu
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe.
Li Yuanchao, anaanza ziara ya siku mbili Zanzibar inayoanza leo.
Kiongozi huyo atawasili katika uwanja wa
ndege wa kimataifa wa Zanzibar saa 10:15 jioni
na kupokelewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Balozi Seif
Ali Iddi.
Mhe.Yuanchao ambae atawasili nchini akitokea
Dar es Salaam, baada ya kufika atakwenda
moja kwa moja Vuga kufanya mazungumzo na timu ya madaktari wa Kichina wanaotoa
huduma katika hospitali za Zanzibar.
Baadae ataelekea Nungwi ambako atapata fursa
ya kuzungumza na Balozi Seif , mazungumzo ambayo yatafanyika hoteli ya
Lagema na baadae kuhudhuria chakula cha
jioni kilichoandaliwa na mwenyeji wake.
Kesho atatembelea mashamba ya viungo
Kizimbani na baade kutembelea Mji
Mkongwe wa Zanzibar, ambako atatembelea Ngome Kongwe, Baitul- Ajab, soko la
zamani la Watumwa na makumbusho.
Ujumbe wa kiongozi huyo utaondoka nchini saa
6:40 mchana ambapo ataagwa na Balozi Seif Ali Iddi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya watu wa China Li Yuanchao wakwanza kulia akisalimiana na Viongozi mbalimbali wa Zanzibar baada ya kuwasili,katikati ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya watu wa China Bwa.Li Yuanchao akiwa na Mwenyeki wake Makamu wa Pli wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, wakiangalia ngoma ya Utamaduni aina ya Msewe baada ya kuwasili Uwanja wa Ngede wa Kimataifa wa Abeids Amani Karume Zanzibar.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya watu wa China Bwa.Li Yuanchao , akisalimiana na Waziri wa Biashara Zanzibar Mhe Nassor Ahmeid Mazrui
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya watu wa China Li Yuanchao wakwanza kulia akisalimiana na Viongozi mbalimbali wa Zanzibar baada ya kuwasili,katikati ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya watu wa China Li Yuanchao akisalimiana na Madaktari Mabingwa kutoka China wanaofanya Kazi katika Hospitali ya Mnazi Mmoja alipowatembelea katika makazi yao Vuga Zanzibar..
No comments:
Post a Comment