Na Madina
Issa
WAZIRI wa
Ustawi wa Jamii, Vijana, Maendeleo na Watoto Zanzibar, Mhe. Zainab Mohammed
Omar, amewataka wafanyakazi wa wizara yake kutumia lugha nzuri wakati wanapotoa
huduma kwa jamii.
Alisema
kutumia lugha chafu wakati wa kutoa huduma kunasababisha mvutano na wananchi na
ni kitendo kisichokubalika.
Alisema hayo
wakati akikabidhi vyeti kwa wafanyakazi bora wa wizara yake pamoja na
kupongezana kwa kula chakula baada ya bajeti ya wizara hiyo kuidhinishwa na
baraza la Wawakilishi.
Alisema wafanyakazi
wana wajibu wa kuhakikisha wanawahudumia wananchi na kuwapa miongozo
inayostahiki badala ya kuwadharau na kuwatolea lugha chafu.
Aliwahimiza
wafanyakazi kufanya kazi kwa kushirikiana na kusaidiana ili kuiletea mabadiliko
wizara hiyo.
Aliwapongeza
wafanyakazi bora kwa kuchapa kazi na kuwahimiza kuongeza bidii ili kuiongezea
ufanisi wizara hiyo na wao wenyewe.
Mimi Jamani nataka kuuliza Huu Mtindo Wakupika NYALI na KUKU, MANYAMA na Kuwalisha ( ATI) Wafanyakazi Umeanzishwa na Nani?.. Na Nikwasababu Gani ?...
ReplyDeleteKwanini Waanzisher Mtindo huu baada ya Kupita kwa Badgeti zao ?... Hii Sio la Waziri Mmoja tu bali nimemshuhudia Mh. Sefu Ali Iddi akifanya Dhifa kjama hizi kila mwaka au mara kwa mara.... Hivo Ndio tuone kwamba Mawaziri Wanawapenda Wafanya kazi wao au ni kuharibu hela ya Walipa kodi tuu.....
Kwanini Viongozi hawa Wasitoe Hela hiyo kwa mfumo wa Sadaka au zakka kwa wale wanaostahiki na badala yake hupika Nyali na Kuku wakawalisha Watu waliokua sio watendaji wazuri wa kazi zao.. Mawizara yote ya SMZ ina Wajuba Washenzi, na Watukanifu. Nashangaa jinsi ninavoona ubaguzi wa rangi, silka na hata pahala pa mtu anapotoka unavotendeka hapo katika wizara mbali mbali za SMZ...