Na
Bakar Mussa, Pemba
RAIS mstaafu
wa awamu ya sita, Alhaj Dk. Aman Abeid Karume, amewataka wazazi kuongeza ushirikiano
na walimu wa madrasa ili kuwaendeleza watoto katika kuhifadhi na kusoma Quran.
Alisema
bila ya ushirikiano lengo la kuendeleza mbele juhudi zinazochukuliwa na waalimu
wa madrasa za kuendeleza dini hiyo hazitazaa matunda.
Aliyasema
hayo katika msikiti wa Ijumaa wa Miembeni Chake Chake kisiwani Pemba,wakati
akizungumza na walimu, wazazi na wanafunzi, walioshiriki mashindano ya kuhifadhi
Quran ambapo alikuwa mgeni rasmi.
Aliwapongeza
walimu waliofanya kazi ya kuwaandaa watoto katika suala zima la kuhifadhi
Quran, kwa vile kazi walioifanya ni kubwa na inataka ujasiri na ustahamilivu.
Alisema
wanachokifanya walimu hao ni muendelezo wa historia ya Zanzibar kuwa itovu cha elimu
ya dini na dunia.
Aliwataka
walimu kuwa kitu kimoja kuliendeleza hilo na kuwataka wengine kuisoma historia
ya Zanzibar ili waone jinsi Wazanzibari
walivyoanza kuwa chem chem ya elimu.
Aliwataka
viongozi kumaliza changamoto zinazowakabili kwani matatizo ni sehemu ya maisha
ya jamii.
Aliwasihi
wanafunzi kuwa tayari kujiendeleza na kwa wale ambao walishindwa basi
wasivunjike moyo wajitahidi kwa mara nyengine kwani wanapoisoma dini yao
matunda yake watayaona.
Mapema
akisoma risala ya jumuiya hiyo, kiongozi wa jumuiya hiyo, Nassor Abdalla Nasor,
alisema jumuiya inakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo ukosefu wa ofisi na vitendea kazi.
No comments:
Post a Comment