Na Khamis Amani
KWA mara nyengine tena, kijana Abdallah Mohammed
Kangoma (38) mkaazi wa Donge Mtambile wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja,
aliyeshitakiwa kwa kumuua mkewe, Msikitu Juma Ali anaendelea kusota rumande baada
ya upelelezi wa kesi hiyo ukiwa bado haujakamilika.
Hayo yamebainika mbele ya Mrajisi wa mahakama kuu,
George Joseph Kazi, wakati mshitakiwa huyo alipofikishwa mahakamani hapo
kuendelea na kesi ya mauaji inayomkabili.
Mshitakiwa aliwasili mahakamani hapo akitokea
rumande ya chuo cha mafunzo kilichopo Kilimani mjini Unguja.
Mshitakiwa alirejeshwa tena rumande hadi Julai
31 mwaka huu atakapofikishwa tena mahakamani.
Abdallah Mohammed Juma alidaiwa kumuua kinyama
mke wake kwa kumkata kwa mapanga kwa shaka ya wivu, tukio ambalo lilitokea
Donge Mtambile Oktoba 3 mwaka jana majira ya saa 12:00 za asubuhi.
Alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Oktoba
9 mwaka jana na kusomewa shitaka la kuua kwa makusudi kinyume na vifungu vya 197
na 197 vya sheria namba 6/2004 sheria za Zanzibar.
No comments:
Post a Comment