Habari za Punde

Kesi mauaji ya Donge yashindwa kusikilizwa



Na Khamis Amani
KWA mara nyengine tena, kijana Abdallah Mohammed Kangoma (38) mkaazi wa Donge Mtambile wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja, aliyeshitakiwa kwa kumuua mkewe, Msikitu Juma Ali anaendelea kusota rumande baada ya upelelezi wa kesi hiyo ukiwa bado haujakamilika.

Hayo yamebainika mbele ya Mrajisi wa mahakama kuu, George Joseph Kazi, wakati mshitakiwa huyo alipofikishwa mahakamani hapo kuendelea na kesi ya mauaji inayomkabili.

Mshitakiwa aliwasili mahakamani hapo akitokea rumande ya chuo cha mafunzo kilichopo Kilimani mjini Unguja.

Mshitakiwa alirejeshwa tena rumande hadi Julai 31 mwaka huu atakapofikishwa tena mahakamani.

Abdallah Mohammed Juma alidaiwa kumuua kinyama mke wake kwa kumkata kwa mapanga kwa shaka ya wivu, tukio ambalo lilitokea Donge Mtambile Oktoba 3 mwaka jana majira ya saa 12:00 za asubuhi.

Alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Oktoba 9 mwaka jana na kusomewa shitaka la kuua kwa makusudi kinyume na vifungu vya 197 na 197 vya sheria namba 6/2004 sheria za Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.