Na Mahmoud
Ahmad, Arusha
WAZIRI
wa Fedha, Sada Mkuya,amezitaka nchi za Afrika kutambua kwamba bara lao ndilo
linalotupiwa macho na dunia kuwa sehemu yenye uhakika wa maisha yao ya siku za usoni.
Aidha
alisema Afrika ni kituo kikubwa cha
shughuli zote za uchumi wa dunia kutokana na kuwepo kwa rasilimali ambazo bado hazijatumika.
Alisema
hayo alipokuwa akifungua mkutano wa wadau wa kodi za ndani kwa nchi za Afrika,
unaoendelea jijini Arusha lengo likiwa ni kubadilishana mawazo, uzoefu na
namna ya ukusanyaji wa kodi kwa maendeleo ya nchi washirika.
Alitaja
baadhi ya rasilimali zilizogundulika kuwa ni pamoja na gesi asilia na mafuta
yanayotarajiwa kuanza kupatikana miaka michache ijayo.
Alisema
kutokana na hali hiyo nchi za bara hilo zinapaswa kujitambua na kuweka
miundombinu mizuri itakayowezesha kuvunwa rasilimali hizo kwa faida ili ziwanufaishe
na kinua uchumi wa nchi zao.
Alitaja
miundombinu hiyo kuwa ni pamoja na
usafiri wa aina zote na elimu ya uvunaji
wa rasilimali hizo ili kuepuka kutafuta wataalamu kutoka nje.
Alisema
baada ya upande huo kuimarika,mikakati mizuri inapaswa kuandaliwa kudhibiti
kodi za ndani ikiwa ni pamoja na kuzuia misamaha ya kodi ambayo imeonekana kuwa
kikwazo katika ukuaji wa pato la nchi.
Alisema
katika kuondoa misamaha ya kodi, nchi hizo zinapaswa kuweka kiwango maalumu cha
misamaha ya kodi badala ya ilivyo sasa ambapo kila nchi inafanya itakavyo.
Aliagiza
wanasiasa kushirikishwa zaidi katika mikutano kama hiyo kwa lengo la kuongeza
uelewa wa masuala ya kodi pamoja na kuwasilisha maoni ya wananchi wao kwa kuwa
yapo mambo yanayoigusa jamii.
Naye Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, Rished Bade, alisema nchi nyingi za Afrika
zinakwama katika ukusanyaji wa kodi kutokana na kuwa na sera mbovu.
Alionya
dhana ya misamaha ya kodi kama njia ya kuwavutia wawekezaji na kuzitaka nchi
hizo kuwa makini akisema misamaha hiyo
ikizidi inaweza kuwa kikwazo na kusababisha nchi hizo kukusanya kodi zake chini
ya viwango.
Hata
hivyo, alisema Tanzania imefanya vizuri katika ukusanyaji wa kodi za ndani
kutokana na mifumo mbalimbali inayotumika hali iliyosababisha kuwa kinara kwa
nchi hizo hadi nchi zingine kuja kujifunza.
No comments:
Post a Comment