Na Haji
Nassor, Pemba
FAMILIA
maskini kisiwani Pemba, ambazo zinawezeshwa kifedha na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
Tanzania (TASAF) awamu ya tatu, zimekumbushwa kuwa fedha wanazopatiwa sio kwa
ajili ya kununulia madira na sare za harusini na badala yake wazitumie kwa
kujikwamua na umaskini.
Kauli
hiyo imetolewa na Muwezeshaji wakati wa ugawaji wa fedha hizo, shehia ya
Ndagoni wila
ya ya Chake Chake, Salma Haji Khamis, kabla ya ugawaji wa fedha
hizo kwa kaya maskini 351.
Alisema
ni vyema wakajipanga ili kuhakikisha fedha hizo zinawaendeleza na kuwakomboa
kutoka kwenye hali ngumu ya umaskini.
“Jamani
fedha tunazaowapa nyinyi kutoka TASAF, mzitumie vyema ikiwa ni pamoja na
kujikusanya pamoja kuanzisha miradi midogo midogo, ambayo inaweza kuwaendeleza
hata baada ya TASAF kumaliza,” alisema.
Aliwataka
wananchi hao kuachana na tabia iliozuka kwa baadhi ya shehia, kuzihonga kamati
zenye kazi ya kuibua kaya maskini kwani kuafnya hivyo sio sahihi.
Nae
Mratibu wa TASAF Pemba, Mussa Said Kisenge, alisema mfuko huo una lengo la
kuwakomboa wananchi maskini, hivyo ni vyema wanapokabidhiwa fedha wazitumie kwa
malengo yaliokusudiwa.
Alisema
zoezi la kutoa fedha hizo kwa awamu hii, lilianza kwa shehia tano za wilaya ya Mkoani
ikiwa ni pamoja na shehia ya Makoongwe, Jombwe, Shamiani, Shidi na Mtangani.
Kwa
wilaya ya Chake Chake shehia ambazo zilikabidhiwa fedha hizo ni Ndagoni kaya 351,
ambazo zilikabidhiwa shilingi 9,405,563,
Kiboni kaya 236 ilikabidhiwa shilingi 5,999,311, Mvumoni kaya 212, shilingi
6,511,769 na Wawi ambapo kuna kaya 251, ambapo zilikabidhiwa shilingi 7,431,060
milioni.
No comments:
Post a Comment