Na
Fatina Mathias,Chemba
KATIKA
hali isiyo ya kawaida, imani za kishirikiana katika baadhi ya maeneo ya halmashauri
ya Chemba mkoani Dodoma, zimetajwa kuwa ni chanzo cha kukwamisha utekelezaji miradi
ya maji na umeme kufuatia wakandarasi kukumbana na vioja mbali mbali ikiwemo
nyoka kila wanapochimba.
Kauli
hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, katika zoezi la kutia saini
mikataba ya ujenzi wa mifumo ya usambazaji maji katika vijiji vitano vya wilaya
hiyo.
Alisema
wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo wanakumbana na hali hiyo kila
wanapofukua mashimo ya kuweka nguzo za
umeme kutoa nyoka badala ya mchanga na kwa upande wa maji maji mabomba yanapasuka muda mfupi baada ya
kufukiwa ardhini kwa madai kuwa wakandarasi hao hawajawashirikisha wazee wa
kimila kabla ya miradi kuanza.
Aliwataka
wakandarasi kuhakikisha wanawaona wazee
wa vijiji hivyo ili kuepuka matukio kama hayo kuendelea kujitokeza na hivyo
kuchelewesha maendeleo kwa wananachi.
“Mambo
ya kimila jamani ni muhimu naomba tuyafuate ili tuondokane na hali hii, wewe
mkandarasi ukawakusanye wazee wa eneo husika unawanunulia mbuzi na pombe ili
wafanye tambiko uweze kufanikiwa
katika
utekelezaji wako,”alisema.
Aidha
aliishukuru serikali kwa kutoa fedha kiasi cha shilingi bilioni 1.187 ikiwa ni
utekelezaji wa mpango wa matokeo makubwa sasa (BRN) katika vijiji vitano.
“Wakazi
hawa wenye shida ya maji watawapa ushirikiano ili kuondokana na vikwazo vya
aina yoyoe na miradi izingatie thamani ya fedha,” alisema.
Kwa
upande wake, Kaimu mhandisi wa maji wa wilaya hiyo, Robert Mganga,alikiri
kuwepo kwa matukio ya aina hiyo na kudai yamekuwa yakikwamisha utekelezaji wa
miradi hiyo.
Naye
Mhandisi wa wakala wa umeme vijijini (REA) Onesmo Kilamuhama, alisema wamekuwa
wakilazimika kufanya matambiko mara kwa mara na wazee wa kimila ili kupata
ridhaa ya kutekeleza mradi huo.
Akizungumza
katika zoezi hilo,Mkuu wa wilaya hiyo, Francis Isaac,alisema wilaya hiyo
inakabiliwa na uhaba wa maji ambapo asilimia 66 ya wananchi hawapati maji
kabisa hali inayochangia kushindwa kushiriki
katika shughuli za maendeleo.
Naye
Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo,William Mafwere, alisema vijiji vitakavyonufaika
na mradi huo ni pamoja na Waida,Chase,Lihonde
na Kisande.
No comments:
Post a Comment