Na Said
Abdulrahman, Pemba
WATU sita
wamefariki dunia katika matukio mbali mbali za ajali yaliyotokea mkoa wa kaskazini Pemba, kuanzia
Januari hadi Juni mwaka huu.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake, Mkuu wa kitengo cha usalama barabarani
mkoani humo, Khalid Ali Gulam, alisema vifo hivyo vilisababishwa na ajali sita
ambapo mbili zilitokea wilaya ya Micheweni na nne wilaya ya Wete.
Aidha
alisema katika ajali hizo watu 19 walijeruhiwa wakiwemo wanawake wanane.
Alisema
katika kipindi hicho polisi walifanya operesheni 10 na kukamata vyombo 132
vikiwa na makosa mbali mbali.
No comments:
Post a Comment