Habari za Punde

Sita wafa ajilini


Na Said Abdulrahman, Pemba

WATU sita wamefariki dunia katika matukio mbali mbali za ajali  yaliyotokea mkoa wa kaskazini Pemba, kuanzia Januari hadi Juni mwaka huu.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake, Mkuu wa kitengo cha usalama barabarani mkoani humo, Khalid Ali Gulam, alisema vifo hivyo vilisababishwa na ajali sita ambapo mbili zilitokea wilaya ya Micheweni na nne wilaya ya Wete.

Aidha alisema katika ajali hizo watu 19 walijeruhiwa wakiwemo wanawake wanane.

Alisema katika kipindi hicho polisi walifanya operesheni 10 na kukamata vyombo 132 vikiwa na makosa mbali mbali.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.