Na Joseph
Ngilisho,Arusha
TANZANIA
itakuwa mwenyeji wa mkutano mkuu wa 45 wa Umoja wa Wabunge wa nchi wanachama wa
Jumuiya ya Madola,kanda ya Afrika (CPA), utakaofanyika Julai 24 hadi 26 mwaka
huu,jiji Arusha.
Aidha
mkutano huo utatanguliwa na vikao mbali mbali kikiwemo cha kamati tendaji,mkutano
wa umoja wa wanawake wa jumuia hiyo,mkutano wa Makatibu wa Mabunge na vikao vya
kanda za mashariki,magharibi,kusini na Afrika ya kati,vitakavyoanza leo.
Akizungumza
na vyombo vya habari Rais wa CPA ambaye pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania,Anne Makinda,alisema bunge la Tanzania limepewa heshima ya kuwa
mwenyeji wa mkutano huo utakaofunguliwa na Rais Jakaya Kikwete na kwamba nchi
18 wanachana zinatarajia kuhudhuriwa,huku washiriki wapatao 500 wakitarajiwa kushiriki.
Alisema
washiriki wa mkutano huo watatoka katika nchi za Botswana, Cameroon, Ghana, Kenya,
Mauritius, Msumbiji, Lesotho, Nigeria, Shelisheli, Namibia, Rwanda, Uganda, Sierra
Leone, Afrika Kusini,Swaziland,Zambia na wenyeji Tanzania.
Alisema
kwamba lengo la mkutano huo ni kupitisha mpango mkakati wa umoja huo kwa kanda
ya Afrika, ambapo moja ya vipengele vyake muhimu ni kubariki ujenzi wa jengo la
kisasa la ofisi
za
kitega uchumi cha umoja huo,kinachotarajiwa kujengwa Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Aliongeza
kuwa wabunge hao watakuwa na fursa ya kubadilishana uzoefu,kujadili changamoto
na mafanikio katika utekelezaji wa majukumu yao ya kikatiba ya kutunga
sheria,uwakilishi na usimamizi wa shughuli za serikali pamoja na kutazama
masuala ya uchaguzi katika nchi hizo.
Alisema
mkutano huo utaangazia masuala ya unyanyasaji wa kijinsia, jinsia katika nyanja
za uchaguzi na kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiuchumi zinazozikabili
nchini wanachama.
Katika
mkutano huo rais wa sasa wa umoja huo,Anne Makinda, atakabidhi rasmi wadhifa
huo kwa Spika wa Lesotho,Sephiri Motanyane.
No comments:
Post a Comment