Habari za Punde

Waislamu watahadharishwa

Na Fatina Mathias, Dodoma
KUMEIBUKA kundi la watu wanaowapotosha Waislamu kwa kuwataka wasiwapeleke watoto wao skuli na vyuo vikuu na  badala yake wasome Quran pekee, kwa madai kwamba elimu ya vyuo vikuu ni ukafiri.
Hayo yalielezwa jana na Mhadhiri wa Dini ya Kiislamu, Dk. Seif Sulley, wakati akizungumza na wakazi wa mjini Dodoma.
Aidha alisema kundi hilo limekuwa likiwahamasisha wanafunzi wa kiislamu walio vyuo vikuu kukatisha masomo yao.
"Kwa gharama yoyote ile nitajitahidi kupambana na kundi hili ambalo linaharibu maisha ya watu,” alisema.
Alisema watu hao wamekuwa wakipita vyuoni na kutoa kauli kama hizo misikitini na kuwaachisha masomo wanafunzi.

Aliwataka Waislamu kuwapiga vita watu hao kwa sababu hawana nia njema na Waislamu na wanapotosha Uislamu ambao umehimiza watu kusoma.

1 comment:

  1. Hao wanaofanya hivo Watakua Sio Waislamu Halisi bali ni Fanatical au Foundamentalistic muslim kama wale WATALABANI.... Quiran imeweka wazi kwamba Muislamu anatakiwa apate Elimu ya Dini na Dunia hata kama Elimu hiyo itakua inatolewa mbali na kutaja mfano wa umbali huo kua ni Uchina.

    Sasa hao Wanaokuja nakuwatia maneno Wazee kwamba watoto wasisome Elimu ya Dunia kwani ni Ukafiri.. Hao watoto wanaweza kupata kazi kweli na kuongoza Nchi yao ikiwa hawana Elimu nyengine baada ya elimu ya dini tuu.....

    Tunatakiwa Watanzania Waislamu tusiwe wajinga kiasi hicho, na tutizame mfano mmoja ambao unaendelea kutokea katika Nchi ya Tanganyika.. Ni kwamba Nafasi zote kubwa za Serikali na Nyeti zimekua zikihodhiwa na Wakristo watupu hali yakua Waislamu wenye Elimu wapo.. Lakini Huu umekua ni Ubaguzi wa Mfumo Kristo wa Serikali ya Tanzania/ Tanganyika...

    Sasa Wanapokuja Muslim Fanatical wakasema tusiwapeleke watoto mashule na badala yake tuwasomeshe Quran tupu..Hivo si tutazidi Kukosa hizo nafasi za uongozi katika Nchi?....

    Mimi nawaomba Waislamu Wasome hata kozio za Upailot na Nyengine ambazo zinakua ni Gender..Muislamu anatakiwa kupata Elimu ya Dini na Dunia Kurani katika Sura til "Ikra" imesema hivo...

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.