Na Kadama Malunde,Shinyanga
UKOSEFU
wa wodi za kutosha katika kituo cha afya cha Kambarage manispaa ya Shinyanga, umesababisha
wanawake wajawazito na waliojifungua kulala wawili katika kitanda kimoja.
Aidha
wengine wanalazimika kuweka magodoro sakafuni hali ambayo inahatarisha afya zao
na watoto wachanga.
Hayo
yalielezwa jana na daktari anayesimamia kituo hicho, Costantine Hubby, wakati
akisoma risala kwa Katibu Mkuu wa Umoja
wa Wanawake Tanzania(UWT), Amina Nassoro Makilagi,baada ya kutembelea kituo
hicho na kujionea jinsi wanawake wanavyoteseka kutokana na ufinyu wa wodi.
Alisema
kituo hicho hakina chumba cha upasuaji wa dharura kwa wajawazito wanaoshindwa
kuzaa kwa njia ya kawaida pamoja na kutokuwa na gari la wagonjwa.
“Kwa sasa tunawachanganya sehemu moja wagonjwa
kwani tuna upungufu wa wodi ya wajawazito na ambao wamejifungua, inabidi walale
chumba kimoja na watoto wao wachanga,”alisema.
Aliiomba
serikali kuboresha mazingira ya vituo vya kutolea huduma kwa kuongeza majengo
na vifaa tiba kwenye zahanati na vituo
vya afya ili kufikia malengo ya millenia.
Akizungumza
na wafanyakazi wa kituo hicho, Katibu Mkuu wa UWT,Amina Makilagi,aliwataka
kuendelea kuwa na moyo wa upendo na uvumilivu wakati wakuhudumia wagonjwa licha
ya kuwepo kwa changamoto nyingi.
Hata
hivyo, aliahidi kufikisha suala hilo kwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii ili
kuona namna ya kuziondoa changamoto hizo.
Kwa
upande wake Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UWT Taifa, Zainab Shomari,
aliwataka wanaCCM kuvunja makundi baada ya uchaguzi kwani ndiyo yanayochangia wananchi wachague viongozi wa upinzani.
No comments:
Post a Comment